HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 11, 2016

DALADALA LAPIGA MWELEKA JIJINI DAR LEO, WATU KADHAA WAJERUHIWA

DALADALA lenye namba za usajili T274 DEX, lililokuwa likifanya safiri zake kati ya Mbagala RangiTatu kuelekea Temeke jijini Dar es Salaam, limepiga mweleka mita chache tu kutoka kituo cha Daladala Sabasaba-Mbagala mapema leo asubuhi (Agosti 11, 2016) na kujeruhi watu kadhaa.

Mashuhuda wanasema, Daladala hilo lililokuwa katika mwendo kasi, liliserereka na kuacha njia wakati likikaribia kusimama kituoni hapo.
Dereva wa Daladala hilo aliruka na kukimbia, nakuwaacha abiria wakitaharuki kila mmoja akijaribu kukoa maisha yake.
“Unajua mvua hizi zilizonyesha asubuhi zinafanya barabara iteleze na hawa jamaa mwendo wao unajua tena, sasa alijaribu kufunga breki gari likaanza kuserereka na alipojaribu kurudi barabarani likakataa na kutumbukia mtaroni,” anasimulia mmoja wa mashuhuda aliyekuwa eneo la ajali.
Polisi wa usalama barabarani alifika muda mfupi baada ya ajali hiyona taratibu ya kuliondoa gari hilo zilianza.
Abiria wote walitoka salama, wachache walijeruhiwa na baadhi yao walionekana wakilia kutokana na mshtuko wa ajali hiyo ya asubuhi.
HABARI/PICHA NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
 Mmoja wa abiria aliyenusurika akilia kwa huzuni kutokana na ajali hiyo
  Mmoja wa abiria aliyenusurika akilia kwa huzuni kutokana na ajali hiyo
 Wapita njia wakimuuliza abiria huyu (aliyekaa), ambaye alikuwa ndani ya daladala hilo
 Polisi wa usalama barabarani, akikagua mazingira ya ajali hiyo huku akizungumza na simu yake ya mkononi
 Mtu huyu ambaye haikujulikana maramoja kama ni muhudumu wa daladala hilo au abiria akitoka ndani ya daladala hilo baada ya "kupiga mwereka'
 Mashuhuda kama kawaida yao

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad