...kazi ya upasuaji ikiendelea maabara
Na Mwandishi Wetu,
Zaidi
ya watoto 50 leo wamehudhuria kambi tiba ya GSM Foundation
inayoendeshwa kwa ushirikiano na Taasisi ya Mifupa na upasuaji ya MOI,
yenye lengo la kupunguza vifo na mtindio wa ubongo kwa watoto
wanaozaliwa na vichwa vikubwa na mgongo wazi, ambayo leo imeingia katika
mkoa wa pili katika msimu wake wa pili pia, wenye lengo la kuwafanyia
upasuaji watoto 100.
Kaimu
Mkuu wa kambi hiyo iliyoanzia mkoani Mtwara Jumanne ya tarehe 2 mwezi
huu, DK Shaaban Hamis, amesema, muiyikio walioupata katika mkoa huu ni
muitikio mkubwa zaidi ukilinganisha na mkoa wa Mtwara, ambako ndio
kunakosadikika kuwa na wagonjwa wengi zaidi, kutokana na rekodi
waliyonayo, baada ya tafiti mbali mbali.
"Inawezekana
hapa tukafanyia upasuaji wagonjwa hata 50 kwa siku hizi tatu
tutakazokuwepo, na labda tukavuka lengo katika mikoa iliyobaki ya Iringa
na Mbeya ambayo ndio ya mwisho katika msimu huu wa pili", alisema Dk
Shaaban.
Kwa
upande wake Afisa uhusiano wa Taasisi ya GSM ambayo kwa mwaka huu
imewekeza zaidi kusaidia sekta ya Afya na Elimu amesema wanafarijika
kuona wagonjwa wanakwenda kutibiwa kama walivyodhamiria, maana ndio
lengo haswa, kusaidia kupunguza vifo vya watoto ambao wanasadikika
kuzaliwa 4000, kwa mwaka lakini kati yao, ni asilimia 25 tu hurudi
hospitalini kwa matibabu huku asilimia 75 wakishindwa kutokana na sababu
za kiuchumi.
Tiba
pekee kwa mtoto mwenye kichwa kikubwa, ama mgongo wazi ni upasuaji,
tiba ambayo gharama zake ni kuanzia shilingi laki tatu za kitanzania,
mpaka milioni moja, kulingana na ubora wa vifaa ama hospitali
anayotibiwa mgonjwa.
Tanzania
ina madaktari Bingwa tisa tu wenye uwezo wa kufanya upasuaji wa namna
hii ambapo nane wanafanya kazi MOI na mmoja anafanya kazi katika
Hospitali ya Bugando jijini Mwanza huku mikoa mingine yote ikiwa haina
madaktari wa namna hii.
Wagonjwa wakisajiliwa katika chumba maalum cha kuwapokea katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma.
Dk Shaaban Hamis, Naibu Mkuu wa Msafara akiwa kazini.
No comments:
Post a Comment