HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, July 12, 2016

AZAM FC CHINI YA WAHISPANIA WAANZA MAZOEZII.

Mtendaji Mkuu wa Azam Fc, Saad Kawemba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KLABU ya Azam FC, ambao tayari wameanza mazoezi yao ya  kujiandaa na msimu ujao (2016-17) ikiwa chini ya benchi jipya la ufundi chini ya makocha kutoka nchini Hispania, linaoongozwa na Zeben Hernandez, Msaidizi wake Yeray Romero, Kocha Mkuu wa Viungo Jonas Garcia na Msaidizi wake, Pablo Borges na Kocha wa Makipa Jose Garcia huku Daktari wa timu, Sergio Perez, akitarajia kutua nchini muda wowote kuanzia sasa.

Mtendaji mkuu wa Azam Fc Saad Kawemba amesema kuwa kwa sasa wapo kwenye mikakati ya kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho kwa kusajili wanne wa kimataifa baada ya Didier Kvaumbagu, Allan Wanga kuondoka. Zaidi pia tunahitaji golikipa wa kimataifa ambaye atasaidiana na Aishi Manula na hasa pia atakuwa msaada kwetu kwenye michuano ya kimataifa na pia hata kweny ligi msimu ujao ambao tunahitaji ubingwa na hilo linawezekana kwani nia ninayo.

"Tunahitaji kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa na hata katika ligi pia ndiyo maana tunataka kufanya usajili utakaokuwa na manufaa kwetu na tumeonelea kwanza tunahitaji golikipa wa kimataifa, beki wa kati na washambuliaji wawili wa kimataifa ambao watachukua nafasi za Kvumbagu na Allan Wanga,"amesema Kawemba. 

Amesema kwa sasa tiulichoamua kingine ni kupandisha vijana wetu wanne kutoka timu ya vijana pia tumefanya mchanganuo wa vikosi kwa sasa Azam watakuwa na vikosi viwili ambapo kila kimoja kitakuwa na wachezaji 22.

Makocha hao wataongezewa nguvu na makocha wengine wazawa waliokuwepo na kikosi hicho msimu uliopita, Kocha Msaidizi Dennis Kitambi na Idd Abubakar, aliyekuwa akiwapata maujuzi makipa wa Azam FC.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad