HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, July 23, 2016

Askari Polisi auawa kwa kapigwa risasi jijini Dar usiku huu

Taarifa iliyotufikia usiku huu, inaeleza kuwa Askari mmoja wa Kikosi cha Usalama Barabarani aliyetambulika kwa jina la Sajenti Mensah wa Kituo cha Polisi cha Oysterbay Kinondoni Jijini Dar es salaam, ameuawa usiku huu kwa kupigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni wahalifu wakati akiwa kazini katika eneo la Sayansi Kijitonyama.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Christopher Fuime amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, ambapo amesema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa mbili usiku huu na chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika.

Taarifa zaidi za zitawajia kadrizitakavyokuwa zikitufikia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad