HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, June 26, 2016

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Wakuu wapya wa Wilaya na afanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Mikoa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.

Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.

Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.

Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali.

Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)


BOFYA HAPO CHINI KUONA MAJINA YA WAKUU WA WILAYA


ARUSHA

1. Arusha - Mrisho Mashaka Gambo
2. Arumeru - Alexander Pastory Mnyeti
3. Ngorongoro - Rashid Mfaume Taka
4. Longido - Daniel Geofrey Chongolo
5. Monduli - Idd Hassan Kimanta
6. Karatu - Therezia Jonathan Mahongo

DAR ES SALAAM
1. Kinondoni - Ally Hapi
2. Ilala - Sophia Mjema
3. Temeke - Felix Jackson Lyaviva
4. Kigamboni - Hashim Shaibu Mgandilwa
5. Ubungo - Hamphrey Polepole

DODOMA

1. Chamwino - Vumilia Justine Nyamoga

2. Dodoma - Christina Solomon Mndeme
3. Chemba - Simon Ezekiel Odunga
4. Kondoa - Sezeria Veneranda Makutta

5. Bahi - Elizabeth Simon
6. Mpwapwa - Jabir Mussa Shekimweli
7. Kongwa - John Ernest Palingo
 

GEITA

1. Bukombe - Josephat Maganga
2. Mbogwe - Matha John Mkupasi
3. Nyang'wale - Hamim Buzohera Gwiyama
4. Geita - Herman C. Kipufi
5. Chato - Shaaban Athuman Ntarambe

IRINGA
 

1. Mufindi - Jamhuri David William
2. Kilolo - Asia Juma Abdallah
3. Iringa - Richard Kasesela
 

KAGERA
 

1. Biharamulo - Saada Abraham Mallunde
2. Karagwe - Geofrey Muheluka Ayoub
3. Muleba - Richard Henry Ruyango
4. Kyerwa - Col. Shaban Ilangu Lissu
5. Bukoba - Deodatus Lucas Kinawilo
6. Ngara - Lt. Col. Michael M. Mtenjele
7. Missenyi - Lt. Col Denis F. Mwila

KATAVI
 

1. Mlele - Rachiel Stephano Kasanda
2. Mpanda - Lilian Charles Matinga
3. Tanganyika - Saleh Mbwana Mhando

KIGOMA

1. Kigoma - Samsoni Renard Anga
2. Kasulu - Col. Martin Elia Mkisi
3. Kakonko - Col. Hosea Malonda Ndagala
4. Uvinza - Mwanamvua Hoza Mlindoko
5. Buhigwe - Col. Elisha Marco Gagisti
6. Kibondo - Luis Peter Bura

KILIMANJARO
 

1. Siha - Onesmo Buswelu
2. Moshi - Kippi Warioba
3. Mwanga - Aaron Yeseya Mmbago
4. Rombo - Fatma Hassan Toufiq
5. Hai - Gelasius Byakanwa
6. Same - Rosemary Senyamule Sitaki

LINDI

1. Nachingwea - Rukia Akhibu Muwango
2. Ruangwa - Joseph Joseph Mkirikiti
3. Liwale - Sarah Vicent Chiwamba
4. Lindi - Shaibu Issa Ndemanga
5. Kilwa - Christopher Emil Ngubiagai

MANYARA
 

1. Babati - Raymond H. Mushi
2. Mbulu - Chelestion Simba M. Mofungu
3. Hanang' - Sara Msafiri Ally
4. Kiteto - Tumaini Benson Magessa
5. Simanjiro - Zephania Adriano Chaula

MARA
 

1. Rorya - Simon K. Chacha
2. Serengeti - Emile Yotham Ntakamulenga
3. Bunda - Lydia Simeon Bupilipili
4. Butiama - Anarose Nyamubi
5. Tarime - Glodious Benard Luoga
6. Musoma - Dkt. Vicent Anney Naano

MBEYA

1. Chunya - Rehema Manase Madusa
2. Kyela - Claudia Undalusyege Kitta
3. Mbeya - William Ntinika Paul
4. Rungwe - Chalya Julius Nyangidu
5. Mbarali - Reuben Ndiza Mfune

MOROGORO

1. Gairo - Siriel Shaid Mchembe
2. Kilombero - James Mugendi Ihunyo
3. Mvomero - Mohamed Mussa Utali
4. Morogoro - Regina Reginald Chonjo
5. Ulanga - Kassema Jacob Joseph
6. Kilosa - Adam Idd Mgoyi
7. Malinyi - Majula Mateko Kasika

MTWARA

1. Newala - Aziza Ally Mangosongo
2. Nanyumbu - Joakim Wangabo
3. Mtwara - Dkt. Khatibu Malimi Kazungu
4. Masasi - Seleman Mzee Seleman
5. Tandahimba - Sebastian M. Walyuba

MWANZA

1. Ilemela - Dkt. Leonald Moses Massale
2. Kwimba - Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon
3. Sengerema - Emmanuel Enock Kipole
4. Nyamagana - Mary Tesha Onesmo
5. Magu - Hadija Rashid Nyembo
6. Ukerewe - Estomihn Fransis Chang'ah
7. Misungwi - Juma Sweda

NJOMBE

1. Njombe - Ruth Blasio Msafiri
2. Ludewa - Andrea Axwesso Tsere
3. Wanging'ombe - Ally Mohamed Kassige

4. Makete - Veronica Kessy

PWANI


1. Bagamoyo - Alhaji Majid Hemed Mwanga
2. Mkuranga - Filberto H. Sanga
3. Rufiji - Juma Abdallah Njwayo
4. Mafia - Shaibu Ahamed Nunduma
5. Kibaha - Asumpter Nsunju Mshama
6. Kisarawe - Happyness Seneda William
7. Kibiti - Gulamu Hussein Shaban Kifu

RUKWA

1. Sumbawanga - Dkt. Khalfan Boniface Haule
2. Nkasi - Said Mohamed Mtanda
3. Kalambo - Julieth Nkembanyi Binyura

RUVUMA

1. Namtumbo - Luckness Adrian Amlima
2. Mbinga - Cosmas Nyano Nshenye
3. Nyasa - Isabera Octava Chilumba
4. Tunduru - Juma Homela
5. Songea - Polet Kamando Mgema

SHINYANGA

1. Kishapu - Nyambonga Daudi Taraba
2. Kahama - Fadhili Nkulu
3. Shinyanga - Josephine Rabby Matiro

SIMIYU

1. Busega - Tano Seif Mwera
2. Maswa - Sefu Abdallah Shekalaghe
3. Bariadi - Festo Sheimu Kiswaga
4. Meatu - Joseph Elieza Chilongani

5. Itilima - Benson Salehe Kilangi

SINGIDA

1. Mkalama - Jackson Jonas Masako
2. Manyoni - Mwembe Idephonce Geofrey
3. Singida - Elias Choro John Tarimo
4. Ikungi - Fikiri Avias Said
5. Iramba - Emmanuel Jumanne Luhahula

SONGWE

1. Songwe - Samwel Jeremiah
2. Ileje - Joseph Modest Mkude
3. Mbozi - Ally Masoud Maswanya
4. Momba - Juma Said Irando
 

TABORA

1. Nzega - Geofrey William Ngudula
2. Kaliua - Busalama Abel Yeji
3. Igunga - Mwaipopo John Gabriel
4. Sikonge - Peres Boniphace Magiri
5. Tabora - Queen Mwashinga Mlozi
6. Urambo - Angelina John Kwingwa
7. Uyui - Gabriel Simon Mnyele

TANGA

1. Tanga - Thobias Mwilapwa
2. Muheza - Mhandisi Mwanaisha Rajab Tumbo
3. Mkinga - Yona Lucas Maki
4. Pangani - Zainab Abdallah Issa
5. Handeni - Godwin Crydon Gondwe
6. Korogwe - Robert Gabriel
7. Kilindi - Sauda Salum Mtondoo
8. Lushoto - Januari Sigareti Lugangika

Wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wanapaswa kufika Ikulu Dar es salaam siku ya Jumatano tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi kwa ajili ya kiapo cha maadili ya uongozi na maelekezo mengine kabla ya kuapishwa na wakuu wa mikoa watakaporejea katika mikoa yao.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
26 Juni, 2016

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad