NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maonyesho ya taasisi za kifedha (benki) na kiuchumi yatakayofanyika Julai 27 hadi 29 mwaka huu, Mlimani City jijini Dar es salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Imori International ambao ndio waandaaji wa Maonyesho hayo, Leo Nyanduga amesema kuwa maonyesho ni kwa ajili ya wananchi kutambua umuhimu wa benki katika kusaidia ukuaji wa uchumi kutokana na fursa zinazozalishwa na benki na taasisi za uchumi.
Nyanduga amesema katika maonyesho hayo fursa mbalimbali za kibiashara zilizopo, mipango ya uwekezaji, pamoja na changamoto zinazoikabili sekta hiyo na kukaa pamoja na kujua ni kwa jinsi gani wanaweza kuzitazama na kuzitatua changamoto hizo.
Amesema maonesho ni kuangalia nafasi ya kuinua maisha ya wananchi katika kuhakikisha wanafaidika kupitia taasisi za kifedha katika kuweza kukopa na kuweza kuwekeza katika miradi mbalimbali.
Nyanduga amesema ni asilimia ndogo ya Watanzania ndiyo wamekuwa wakitumia huduma za kibenki kutokana na kukosa elimu ya kutosha ya faida za kutumia sekta za benki na uwekezaji katika soko la hisa, lakini kupitia Maonyesho hayo ya Taasisi za Kibenki 2016 wengi watafaidika.
Amesema wananchi watapata nafasi ya kupata elimu na kukutana kwa karibu na watumishi wa mabenki, soko la hisa, vicoba, microfinance, huduma za kifedha kupitia mitandao ya simu na kujenga ukaribu ili kuhakikisha wananchi wanatumia kikamilifu huduma zao katika kusaidia ukuaji wa sekta ya fedha nchini.
Nyanduga ameeleza kuwa maonyesho hayo ya sekta za kifedha na uchumi yaliyodhamiria kuwa chachu kuu ya kukutanisha benki zote, taasisi zote za kifedha, taasisi zote zinazoweza kutoa huduma mbalimbali kwenye sekta hiyo, yatakuwa ni mwanzo wa kukuza zaidi sekta hiyo kikamilifu.
Amesema maonyesho yaleta chachu katika sekta, kuwapa nafasi watu kujua namna taasisi hizi za kifedha zinavyoweza kutatua changamoto zao wakizitumia vyema.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Imori International ambao ndio waandaaji wa Maonyesho hayo, Leo Nyanduga amesema kuwa maonyesho ni kwa ajili ya wananchi kutambua umuhimu wa benki katika kusaidia ukuaji wa uchumi kutokana na fursa zinazozalishwa na benki na taasisi za uchumi.
Nyanduga amesema katika maonyesho hayo fursa mbalimbali za kibiashara zilizopo, mipango ya uwekezaji, pamoja na changamoto zinazoikabili sekta hiyo na kukaa pamoja na kujua ni kwa jinsi gani wanaweza kuzitazama na kuzitatua changamoto hizo.
Amesema maonesho ni kuangalia nafasi ya kuinua maisha ya wananchi katika kuhakikisha wanafaidika kupitia taasisi za kifedha katika kuweza kukopa na kuweza kuwekeza katika miradi mbalimbali.
Nyanduga amesema ni asilimia ndogo ya Watanzania ndiyo wamekuwa wakitumia huduma za kibenki kutokana na kukosa elimu ya kutosha ya faida za kutumia sekta za benki na uwekezaji katika soko la hisa, lakini kupitia Maonyesho hayo ya Taasisi za Kibenki 2016 wengi watafaidika.
Amesema wananchi watapata nafasi ya kupata elimu na kukutana kwa karibu na watumishi wa mabenki, soko la hisa, vicoba, microfinance, huduma za kifedha kupitia mitandao ya simu na kujenga ukaribu ili kuhakikisha wananchi wanatumia kikamilifu huduma zao katika kusaidia ukuaji wa sekta ya fedha nchini.
Nyanduga ameeleza kuwa maonyesho hayo ya sekta za kifedha na uchumi yaliyodhamiria kuwa chachu kuu ya kukutanisha benki zote, taasisi zote za kifedha, taasisi zote zinazoweza kutoa huduma mbalimbali kwenye sekta hiyo, yatakuwa ni mwanzo wa kukuza zaidi sekta hiyo kikamilifu.
Amesema maonyesho yaleta chachu katika sekta, kuwapa nafasi watu kujua namna taasisi hizi za kifedha zinavyoweza kutatua changamoto zao wakizitumia vyema.
No comments:
Post a Comment