HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 27, 2016

MASHABIKI 40,000 KUWAONA.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KIKOSI cha Yanga kipo tayari kuwavaa TP Mazembe kesho katika mchezo wa pili wa kombe la Shirikisho Afrika ambapo unatarajiwa kupigwa katika dimba la uwanja wa Taifa huku wachezaji wote wakiwa katika hali nzuri kimchezo na kisaikolojia. Hayo yamesemwa leo katika mkutano na waandishi wa habari kuwa Wachezaji wapo tayari kwa ajili ua ushindi.

Mkuu wa Kitengo cha habari na Mawasiliano Jerry Muro amesema kuwa, kwa sasa kilichobakia ni kuweza kusubiri muda ufike na kwa maelezo ya kocha mkuu Hans Van De Pluijm amehakikishia wanachama wa Yanga kuwa watapambana hadi hatua ya mwisho." Kocha mkuu amesema kuwa wachezaji wote wapo sawa na watapambana hadi hatua ya mwisho na wamewahakikishia benchi la ufundi kuwa wapo uwanja wa nyumbani na watautumia vizuri,".
Muro amesema kuwa, msimamizi wa mechi hiyo amewataka viongozi wa Yanga kuhusiana na mechi ya kesho katika 
uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwa  una uwezo wa kuchukua watu 60,000, lakini kesho utafungwa wakati wa mchezo wa Yanga na TP Mazembe ya DRC baada ya mashabiki 40,000 kuingia.

Hayo ni maagizo ya Kamisa wa mchezo huo wa Kundi A Kombe la Shirikisho Afrika, ambao mashabiki wataingia bure, Celestine Ntangungira kutoka Rwanda.

Sasa Mabingwa hao wa Tanzania Bara watashuka kuja kupigana kuonyesha hawapotez mchezo wa nyumbani hata mmoja hasa baada ya ule wa awali kupoteza nchini Algeria.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad