Mkurugenzi
wa kampuni ya Ovans Construction Company Limited, ambao ni wamiliki wa
Kusile Restaurant and Lodge, Valence Urio upande wa kulia akiwa ameshika
Mwenge wa Uhuru mara baada ya Kiongozi wa mbio za Mwenge George Mbijima
kufungua rasmi hoteli hiyo iliyopo Mbinga mjini mkoani Ruvuma. Ni Hoteli ya kisasa iliyopo Mbinga mjini mkoani Ruvuma ikiwa ni Hotel ya kwanza na ya kisasa katika wilaya hiyo
Msimamizi
wa hoteli ya Kusile Restaurant and Lodge, Mary Thomas upande wa kushoto
akisoma taarifa ya maendeleo juu ya ujenzi wa hoteli hiyo ya kisasa kwa
Kiongozi wa mbio za Mwenge, George Mbijima wa pili kutoka kulia. Wa
pili kutoka kushoto ni mmiliki wa hoteli hiyo,
Verena Urio. Mradi huu
umefanikiwa pia kuwawezesha wakulima wadogo wadogo 10 kuanzisha kilimo cha
mboga mboga maalumu ambazo hazipatikani Mbinga, hivyo kutengeneza soko la
uhakika kwa mboga mboga hizo na zile za kawaida pia imefanikiwa kutengeneza ajira 22 ambapo kati ya hizo
wanawake wapo 16 na wanaume sita.
Kiongozi
wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, George Mbijimi akiondoa kitambaa
ikiwa ni ishara ya ufunguzi rasmi wa hoteli ya kisasa ya Kusile
Restaurant and Lodge iliyopo Mbinga mjini mkoani Ruvuma. Ambapo Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge,
aliwataka watoa huduma katika hoteli hiyo wahakikishe kwamba wanatoa huduma
zinazolingana na hadhi ya jengo hilo, ili biashara wanazozifanya ziweze kuwa
endelevu.
Hata hivyo Mbijima amewapongeza wamiliki wa jengo hilo la
biashara, kwa ubunifu walioufanya ambao utasaidia kupunguza uhaba wa nyumba ya
kisasa ya kulala wageni na kuweza kupata huduma bora ya chakula.
Mkurugenzi
wa kampuni ya Ovans Construction Company Limited, ambao ni wamiliki wa
Kusile Restaurant and Lodge, Valence Urio akimwelekeza kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa 2016 George Mbijima
No comments:
Post a Comment