HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, May 28, 2016

WAHADZABE WALALAMIKA KUTENGWA

Na Woinde Shizza, Karatu.

Watu wa Jamii ya Wawindaji waokota matunda na walina asali kutoka kabila la Wahadzabe katika kijiji cha Endamagh wilaya ya Karatu, wamelalamika kitendo cha kutengwa kuingizwa kwenye mpango wa ruzuku kwa kaya masikini, unaoendeshwa na TASAF wakati wao ni jamii masikini zaidi, kwani kati yao ni kaya saba tu ndizo zilizo ingizwa kwenye mpango huo, hivyo wanalazimika kugawana kiasi kidogo wanacho  kipata.

Watu hao wa kabila la Wahadzabe wametoa kauli hiyo  katika kijiji cha Endamash, walipotembelewa na maafisa wa TASAF kutoka Makao Makuu, pamoja na wawakilishi wa Benki ya Dunia, ambapo wamedai sasa wanalazimika kugawana fedha zinazo tolewa kwa kaya saba kwakuwa wote hawana uwezo na matunda na wanyamapori wameadimika kutokana na ukame.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia, Billar Bird amesema amesikitishwa na hali waliyo nayo watu hao, lakini amechukua maombi yao na atayafikisha kwenye kikao cha nchi wafadhili wanaotarajia kukutana mwezi ujao.

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Ladislaus Mwamanga amesema kasoro hizo zimetokana na tabia ya jamii hiyo ya kuhamahama ndiyo maana walikosa fursa hiyo lakini  TASAF itaangalia namna ya kuwasaidia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad