Na Sultani Kipingo
Katika kunogesha Libeneke hili, Globu ya Jamii kuanzia leo linazindua makala mpya maalumu itakayojulikana kama “MULIKA VIJIPU UPELE”, lengo kuu likiwa ni kuanika mambo ya uzembe, kutowajibika, kujisahau, huduma mbovu, kufanya kazi kwa mazoea na madudu mengine mengi yanayokera jamii. Hii ni katika kutoa mchango wetu mdogo katika kuisaidia serikali ya awamu ya tano kuweka mambo sawa.
Katika kunogesha Libeneke hili, Globu ya Jamii kuanzia leo linazindua makala mpya maalumu itakayojulikana kama “MULIKA VIJIPU UPELE”, lengo kuu likiwa ni kuanika mambo ya uzembe, kutowajibika, kujisahau, huduma mbovu, kufanya kazi kwa mazoea na madudu mengine mengi yanayokera jamii. Hii ni katika kutoa mchango wetu mdogo katika kuisaidia serikali ya awamu ya tano kuweka mambo sawa.
Makala hii
itakujia wakati wowote “Vijipu Upele” vitapoonekana popote pale nchini. Na
katika kutekeleza na kufanikisha hili, pia tunakaribisha michango ya picha na
habari kutoka kwenu waheshimiwa wadau wetu. Tuma kwa kupitia email address ya issamichuzi@gmail.com au kwa WhatsApp
namba +255 754 271 266, nasi tutairusha hewani mara moja. Hakikisha unataja
nini, wapi na lini.
Kwa kuanzia
na kama mfano wa zoezi hili, mmulika “Vijipu Upele” wetu ametembelea mji wa Dodoma na kuvinjari katika bustani maarufu ya Nyerere Square, na kukuta wana Dodoma wengi wako pale wakipunga upepo ama utengeneza kucha zao na urembo mwingine ama kupiga picha kama ilivyo ada ya mahali hapo.
Lakini lahaula! Hali aliyoikuta mmulikaji "Vijipu Upele" wetu kwenye mnara wenyewe wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni ya kusikitisha....
Wanasema bandubandu humaliza gogo. Na endapo hakuna juhudi za makusudi za kuuokoa mnara huo hazitafanyika haraka, basi mambo yatakuwa mengine, maana karibu sakafu ya mnarani hapo sio tu inameguka na kuvunjika, bali pia karibu slabs za sakafu yote zimelegea. Hatuna uhakika kwamba tatizo ni kutumika sana kwa watu kutembelea kila siku kwa wingi, ama mafundi waliofanya kazi hiyo alilipua kazi.
Jionee mwenyewe taswira hizi.....
Lakini lahaula! Hali aliyoikuta mmulikaji "Vijipu Upele" wetu kwenye mnara wenyewe wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni ya kusikitisha....
Wanasema bandubandu humaliza gogo. Na endapo hakuna juhudi za makusudi za kuuokoa mnara huo hazitafanyika haraka, basi mambo yatakuwa mengine, maana karibu sakafu ya mnarani hapo sio tu inameguka na kuvunjika, bali pia karibu slabs za sakafu yote zimelegea. Hatuna uhakika kwamba tatizo ni kutumika sana kwa watu kutembelea kila siku kwa wingi, ama mafundi waliofanya kazi hiyo alilipua kazi.
Jionee mwenyewe taswira hizi.....
No comments:
Post a Comment