Mkurugenzi wa Idara ya Bima wa wa Kampuni ya Kimataifa ya Ernest & Young (EY), Sujay Shah akizungumza katika mkutano wa wadau ulioandaliwa na kampuni hiyo wa kujadili ripoti sekta ya bima na umuhimu wake katika nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Kiongozi wa Kanda ya Mashariki wa Idara ya Fedha na Ushauri wa Huduma ya Sekta binafsi wa EY, Steve Osei Mensah akizungumza katika mkutano wa wadau ulioandaliwa na kampuni hiyo wa kujadili ripoti sekta ya bima na umuhimu wake katika nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkazi wa EY Tanzania, Joseph Sheffu akizungumza na waandishi habari juu ya sekta bima iliopo nchini na ukuaji wake katika huduma hiyo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii.
Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
WADAU wa sekta ya Bima wamesema kuwa Tanzania iko chini kwa matumizi ya bima katika nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara kutokana na kutotambua mchango wa bima katika pato la taifa.
Akizungumza katika mkutano wa Wadau bima ulioandaliwa na wa Kampuni ya Kimataifa ya Ernest & Young (EY), wa kujadili ripoti sekta ya bima na umuhimu wake katika nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara, Mkurugenzi Mkazi EY Tanzania, Joseph Sheffu, amesema kuwa sekta bima iko kama biashara nyingine ya kuchangia pato la Taifa.
Amesema nchi zilizo katika ripoti hiyo ni Uganda, Malawi ,Kenya,Nigeria pamoja na Tanzania, ambapo katika ripoti hiyo Tanzania ni asilimia 0.8 inachangia katka pato la Taifa wa bima zisizo za maisha.
Sheffu amesema wanaotumia bima nchini ni asilimia 0.1 ya watu wote katika pato la Taifa huku Kenya ikiwa na asilimia moja na pamoja Uganda asilimia 0.09.
Amesema kuwa Tanzania kuwa nyuma katika bima ni kutokana historia ya Ujamaa, ugonjwa wa ukimwi ambao ulifanya umri wa kuishi kupungua na bima kushindwa kuwewekeza katika bima ya maisha.
Aidha amesema katika kampuni za bima 27 ni kampuni mbili tu ndio zinatoa bima ya maisha kutokana na watanzania kutojua umuhimu huo kwa kujua mtu hata akifariki family yake itaangaliwa na ndugu zake.
Sheffu amesema katika bima ya maisha Tanzania imefikia na dola sita, Kenya dola 40 na soko la bima lililopo nchini hatumiwi ipasavyo.
No comments:
Post a Comment