HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 27, 2016

Isamilo, Dar Swim Club zatamba kushinda mashindano ya kuogelea ya Tallis

Timu  ya kuogelea ya Isamilo kutoka mkoa wa Mwanza  na Dar Swim Club zimetamba kutwaa nafasi ya kwanza katika mashindano ya  kuogelea ya Tallis yaliyopangwa kuanza Ijumaa Januari 29 na kumalizika Jumamosi Januari 30 kwenye bwawa la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika ( IST Upanga).

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Mwanza jana, Mwenyekiti wa Klabu ya  Kuogelea  ya Mwanza (MSC), Jason Miller alisema kuwa wamejiandaa vilivyo kutwaa medali za dhahabu katika mashindano hayo amayo yatafanyika kwa siku mbili.

Miller alisema kuwa klabu ya Isamilo ndiyo  inawakilisha mkoa huo katika mashindano hayo ambayo yanatarajiwa kushirikisha waogeleaji zaidi ya 400 kutoka klabu mbalimbali  hapa nchini.
Peter Itatiro wa Dar Swim Club akionyesha umahiri wake katika kuogelea. Peter ana miaka 9 atashiriki katika aina nne ya mashindano hayo kwa staili zote.

Alisema kuwa wamecagua waogeleaji 21 kwa ajili ya mashindano hayo na kwa muda wote walikuwa katika mazoezi makali. “Najua kuna ushindani mkubwa sana katika mashindano , tulifanya mazoezi kwa muda mrefu na kuwashindanisha staili mbalimbali za kuogelea kwa  kuzingatia muda, wote wameonyesha muda mzuri na tupo tayari kwa mashindano,” alisema Miller.

Aliwataja wachezaji wake kwa upande wa wasichana kuwa ni Anna Guild,  Emma Imhoff,  Bridget  Peck,  Rebecca Guild,  Nandi O’Sullivan,  Natalie Mulford,  Sachi Buggana, Sofia Sanchez,  Isobel Sanchez,  Umi Kulthum na  Maisah Pirani.
Kwa upande wa wavulana ni  Matthew Guild,  Elia Imhoff,  Eric Nixon,  Khaleed Razac, Judah Miller, Caleb O’Sullivan,  Delvin Barick, Jack  Peck,  Daniele Imhoff na  Ezra Miller.

Wakati Isamilo ikitamba, klabu maarufu ya Dar Swim Club nayo imetamba kulibakisha taji la mashindano hayo  kutokana na mazoezi ambayo wameyafanya.

Katibu Mkuu wa Dar Swim Club, Inviolata Itatiro alisema jana kuwa wamejiandaa vilivyo kwa ajili ya kutwaa medali nyingi za zawadi na hasa ukizingatia kuwa waogeleaji wao wana uzoefu wa kimataifa.

Inviolata alisema kuwa hivi karibuni walifanya vyema katika mashindano yaliyofanyika nchini Dubai na kushirikisha waogeleaji kutoka nchi mbalimbali duniani huku wao wakiwa wanashiriki kwa mara ya kwanza.
“Tulishinda medali za dhahabu katika mashindano hayo, waogeleaji wetu wamepata uzoefu mkubwa, naamini watafanya vyema,” alisema Inviolata ambapo jumla ya waogeleaji 50 wataiwakilisha klab hiyo.

Waogeleaji hao ni Meyia Avery, Anna Azzoni, Chinwe Bruns, Joshua Bruns, Isobel Bush, Klaryce Durand, Smriti Gokan, Bailey Golembeski, Carter Golembeski,  Celina Itatiro, Lidia Janik, Ursulla Khimji, Mayli Kiepe, Naaliyah Kweka, Saffiro Kweka, Lois Scheren, Diya Shah, Maya Somaiya, Niki  Somaiya, Kelya Temba, Maia Tumiotto, Lara Van Den Hombergh  na  Chichi Zengeni ambao ni wasichana.
Waogeleaji wa klabu ya Dar Swim Club walifanya mazoezi kwa ajili ya mashindano ya Tallis yaliyopangwa kuanza Ijumaa kwenye bwawa la kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST) Upanga. 

Kwa upande wa wavulana ni  Timothee Callens, Sebastian Carpintero, Raahi Davda, Jean De  Villard, Marin De Villard, Victoire De Villard, Flore De Villeneuve,  Gaspard De Villeneuve, Luwe De Wet, Joaquim Deering, Lisa Di  Stefano,Josh Golembeski,Matt Golembeski, Peter Itatiro, Jonathan, Lubuva, Adrien Madjitoloum, Reuben Monyo, Emmanuele Moroni, Rodolfo Moroni, Thierry Murunga, Christopher Nikitas, Ishaan Patel, Victor  Richmond, Kees Rodenburg, Neel Ruparelia, Arjun Taylor  na  Alessandro Tumiottoends…

Mratibu wa mashindano hayo, Alexander Mwaipasi alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na timu zaidi ya 15 zitashiriki katika mashindano hayo. “Timu nyingi zimetuma majina ya waogeaji wao na zipo tayari kwa mashindano,” alisema Mwaipasi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad