Meneja Mkuu wa kampuni ya Tigo, Diego Gutierrez, akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kwenye mkutano kuhusina na kampuni ya Tigo kuanza kutumia mfumo wa kwanza Afrika wa mawasiliano ya 4G DVNO ikishirikiana na Uhuru One.
Meneja Mkuu wa Tigo,
Diego Gutierrez akiwa na Mwenyekiti wa uhuru One Rajab Katunda wakati wa
uzinduzi kuanzisha kutumia mfumo wa kwanza Afrika wa mawasiliano ya 4G
DVNO ikishirikiana na Uhuru One.
KAMPUNI ya Tigo na kampuni ya UhuruOne wameanzisha ushirikiano
na kuunda mfumo wa utoajihuduma za kimtandao usiotumia miundombinu asilia ya
mawasiliano (Data Virtual Network Operator – DVNO) na ambao utaiwezesha
UhuruOne kupanua upatikanaji wa huduma zake
kwa kutumia teknolojia ya 4G.
Aina hii ya mfumo wa mtandao ni ya kwanza barani
Afrika.
Mfumo wa DVNO utaiwezesha UhuruOne kusambaza taarifa za kimtandao pamoja na mtandao wa data wa Tigo 4G LTE
utakaowezesha wateja wake kutumia data
zilizowezeshwa kupitia kasi kubwa ya 4G.
Akitoa maoni yake kuhusu hili, Meneja Mkuu wa Tigo,
Gutierrez alisema: “Hii ni mara ya kwanza barani kuwepo na ushirikiano wa aina
hii ambapo Tigo inafurahia kufanikisha jambo hili kwa kushirikiana na UhuruOne.
Kuzinduliwa kwa teknolojia ya 4G ni sehemu ya muendelezo wa mkakati wa Tigo
kuboresha ubora huduma zake na kuwafikishia watu wengi zaidi huduma ya
mawasiliano nchini.”
Aidha Mwenyekiti wa UhuruOne Rajabu Katunda
alisema“tunaiona Afrika ikichipua
kiteknolojia, lakini kujumuisha
uwanda mpana wa mawasiliano na dijitali
kwenye uchumi wetu kutautendea uchumi wetu jambo ambalo litatuneemesha
sisi wenyewe na kutuinua kimaisha. Hili ni jambo la kipekee na la kujivunia kwa
UhuruOne ambayo imekuwa katika harakati za ubunifu kupitia mtandao wa intaneti
tangu mwaka 2009 na pia ni mwanachama mwasisi wa Umoja wa Dynamic Spectrum”.
No comments:
Post a Comment