HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 8, 2015

WAGOMBEA WAACHE KUTUMIA UDINI NA UKANDA–NAPE

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye (Pichani) amewataka wagombea wa vyama mbalimbali vya siasa kuacha kutumia Udini au Ukanda kutokana na kufanya hivyo ni kuigawa nchi.
  
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mnauye amesema kuwa kuna watu katika kampeni wamejitokeza kutumia udini na ukanda vitu ambayo ni kinyume na maadili ya uchaguzi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
 
Amesema kuwa baadhi ya wagombea wameonekana katika ibada wakitaka wachaguliwe katika nafasi walizogombea hali ambaya italeta mpasuko wa  udini dhidi ya watu wengine. 
 
AIDHA Nape amesema kuwa kutokana maadili yaliyotolewa na NEC wagombea wafuate katika kuendesha kampeni ambazo haziwagawi watu.
 
“Uchaguzi huu watu wasitumie udini au ukanda kwani unagwa watanzania hivyo kila mtu afanye kampeni za kiistarabu na NEC ichukue hatua kwa watu wanaotumia udini”amesema Nape.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad