HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 21, 2015

WADAU WA DAWA WAKUTANA JIJI DAR ES SALAAM LEO

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donnan Mmbando akizungumza  na waandishi wa habari juu ya matumizi ya dawa  katika Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki yawe na uwiano sawa na kuwa na kiwango kinachokubalika Kimataifa. Amesema  mamlaka husika inapaswa kusimamia na wataalam wa dawa ili kuendana na soko  la Jumuiya ya  Afrika Mashariki, leo Jijini Dar es Salaam
 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Bw. Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu jinsi namna  wananchi watapata dawa zilizo bora na salama zaidi kwa kutumia vigezo vya kikamataifa kwa kuwa kuzingatia masharti yanayotolewa na Shirika la Afya Duniani. Amesema Tanzania ni nchi ya kwanza kutoa uhamasishaji huu kwa wadau  wazalishaji na wasambazaji wa  dawa na wote wanaojihusisha na biashara ya dawa na kwamba  hii ni jumuiya  ya kwanza  katika bara la Afrika kutekeleza mpango wa kuwa na mifumo ya aina moja ya uthibiti wa dawa kwa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 Sehemu ya wadau wa dawa walio hudhulia kikao hicho leo Jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donnan Mmbando na  Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Bw. Hiiti Sillo wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Donnan Mmbando na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Hiiti Sillo wakifurahia jambo baada ya kikao hicho (Picha na Emmanuel Mssaka)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad