HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 23, 2015

UHUSIANO WA MASUALA YA UTAMADUNI KATI YA TANZANIA NA CHINA WAENDELEA KUBORESHWA

 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (katikati) akimsikiliza Afisa Balozi wa China anayehusika na masuala ya Utamaduni nchini Tanzania Bw. GAO WEI (wapili kushoto) walipofika katika ofisi za Wizara kutambulisha uongozi mpya na kutoa nafasi kwa uongozi wa zamani kuaga Wizara yenye dhamana na masuala ya Utamaduni leo Jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (kulia) akimkabidhi Afisa Balozi wa China aliyemaliza muda wake katika masuala ya Utamaduni  nchini Tanzania Bw. LIU DONG zawadi ya picha ya Tingatinga kama ishara ya kumpongeza kwa kuhamasisha mahusiano mazuri ya kiutamaduni kati ya Tanzania na China leo Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga (kulia) akiangalia vitu mbalimbali vya kiutamaduni alivyokabidhiwa na Afisa Balozi wa China aliyemaliza muda wake katika masuala ya Utamaduni nchini Tanzania Bw. LIU DONG (katikati) leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Balozi wa China anayehusika na masuala ya Utamaduni nchini Tanzania Bw. GAO WEI

Picha na: Genofeva Matemu - Maelezo

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad