HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 16, 2015

MBEYA CITY 3, HUKU JKT RUVU MAMA KAJABWELA TUMBO KAMSOKOTA BILAA....

Kocha wa Timu ya Mbeya City fc a.k.a Wakoma Kumwanya ndugu, Juma Mwambusi akizungumza jambo na baadhi ya Vyombo vya Habari mara baada ya Mtanange huo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara kumalizika katika Uwanja wa kumbukumbu Sokoine Jijini Mbeya, Ambapo Mbeya City fc waliibuka kidedea kwa kuichalaza Jkt Ruvu goli 3-0, ambapo Dakika ya 23 mchezaji Joseph Mahundi kuipatia Mbeya City Goli la Kwanza na Goli la Pili toka kwa Temy Felix Dakika ya 57 kwa mkwaju wa Penati, huku Goli la Tatu kufungwa na David Kabole Dakika ya 71.
kiungo wa Mbeya City fc Geofrey Mlawa akiteleza na Mpira katika Mtanange huo uliochezwa katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Kamati ya Ufundi..
Baadhi ya Mashabiki Kinazi wa Timu ya Mbeya City fc wakishangilia katika Mtanange huo wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ambapo Mbeya City waliibuka mshindi kwa goli 3-0...

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad