Mkuu
wa kituo cha Kulelea Watoto yatima cha Al-Madina, Bi. Kulthum Juma
akizungumzia kuhusu kituo hicho pamoja na kutoa shukrani kwa kampuni ya
Multichoice Tanzania kwa kuendelea kukisaidia kituo cha hicho ambacho
kina takribani watoto 68 na pia kituo hicho kipo eneo la Tandale kwa
Tumbo jijini Dar.
Ustadhi Mashaka Salim akitoa neno.
Mkurugenzi wa Multichoice Tanzania, Peter Fauel akichukua chakula wakati wa kuwafuturisha watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha Al-Madina kilichopo Tandale kwa Tumbo, Wa pili kutoka kulia ni Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo.
Meneja
Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi, akitoa
huduma ya chakula kwa watoto yatima hii ikiwa ni njia mojawapo ya
kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu.
Dar es Salaam, Alhamisi 9 Julai 2015: Kampuni ya Bima ya Resolution leo hii imeaanda hafla ya
kufuturisha wateja wake katika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam. Hafla
ilihudhuriwa na Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Musa Bin Salum.
Huu ni mwaka wa pili mfululizo kwa kampuni hiyo ya bima
kushirikiana na wateja wake katika iftar kwa lengo la kuwaleta karibu wateja
wao na kuwashukuru kwa ushirikiano wa mwaka hadi mwaka.
"Tunawashukuru
sana kwa kuhudhuria hafla hii na tunawapongeza kwa uvumilivu wenu katika mwezi
huu mkuu wa Ramadhan.” Meneja Mkuu wa
Resolution Insurance nchini Tanzania, Bwana Oscar Osir alisema.
Katika
hafla hiyo Shiekh Mkuu aliwakumbusha waumini wote umuhimu wa mfungo wa mwezi
mtukufu wa Ramadhan.
“Ningependa
kuwahimiza Waislamu wenzangu kutia maanani amri wakati wa Mwezi Mtukufu.
Tuonesha upendo na uvumilivu kwa wote, kusameheana na kuwasaidia wale ambao
hawana uwezo wa kujisaidia” Sheikh Alhad
alisema.
"Tunashukuru
sana kwa ushirikiano wenu kwani ndiyo inatupa motisha ya kuendelea kuwapa
huduma bora zaidi. Katika shughuli za kuwapa Huduma zilizo bora zaidi na
zinazoweza kuwahudumia ukiwa hapa nchini na hata sehemu yeyote duniani. Ningependa
pia kuwahakikishia kuwa tutaendelea kuwapa bidhaa bora na kuwasikiliza ili
tutimize mahitaji yenu", alisema Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa
Resolution Insurance Bi Zuhura Muro.
Baadhi
ya Watoto yatima, Wafanyakazi wa Multichoice Tanzania pamoja na
viongozi wa kituo hicho cha Al-Madina wakichukua chakula katika futari
iliyoandaliwa na kampuni ya Multichoice Tanzania.
Baadhi
ya Watoto yatima, Wafanyakazi wa Multichoice Tanzania pamoja na
viongozi wa kituo hicho cha Al-Madina wakijumuika katika futari hii
ikiwa ni moja wapo ya kutoa msaada katika vituo mbalimbali hapa nchini.
Meneja
wa Fedha wa Multichoice Tanzania, Francis Senguji akitoa neno la
shukrani kwa niaba ya Kampuni ya Multichoice Tanzania kwa waliofika na
kujumuika nao katika futari iliyoandaliwa na Kampuni ya Multichoice
Tanzania.
No comments:
Post a Comment