HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 10, 2015

DSTV TANZANIA YAFUTURISHA WATOTO YATIMA WA KITUO CHA AL- MADINA

Mkuu wa kituo cha Kulelea Watoto yatima cha Al-Madina, Bi. Kulthum Juma akizungumzia kuhusu kituo hicho pamoja na kutoa shukrani kwa kampuni ya Multichoice Tanzania kwa kuendelea kukisaidia kituo cha hicho ambacho kina takribani watoto 68 na pia kituo hicho kipo eneo la Tandale kwa Tumbo jijini Dar.
Ustadhi Mashaka Salim akitoa neno.
Mkurugenzi wa Multichoice Tanzania, Peter Fauel akichukua chakula wakati wa kuwafuturisha watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha Al-Madina kilichopo Tandale kwa Tumbo, Wa pili kutoka kulia ni Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo.
04
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi, akitoa huduma ya chakula kwa watoto yatima hii ikiwa ni njia mojawapo ya kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu.


Dar es Salaam, Alhamisi 9 Julai 2015: Kampuni ya Bima ya Resolution leo hii imeaanda hafla ya kufuturisha wateja wake katika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam. Hafla ilihudhuriwa na Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Musa Bin Salum.

Huu ni mwaka wa pili mfululizo kwa kampuni hiyo ya bima kushirikiana na wateja wake katika iftar kwa lengo la kuwaleta karibu wateja wao na kuwashukuru kwa ushirikiano wa mwaka hadi mwaka.

"Tunawashukuru sana kwa kuhudhuria hafla hii na tunawapongeza kwa uvumilivu wenu katika mwezi huu mkuu wa Ramadhan.” Meneja Mkuu wa Resolution Insurance nchini Tanzania, Bwana Oscar Osir alisema.

Katika hafla hiyo Shiekh Mkuu aliwakumbusha waumini wote umuhimu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

“Ningependa kuwahimiza Waislamu wenzangu kutia maanani amri wakati wa Mwezi Mtukufu. Tuonesha upendo na uvumilivu kwa wote, kusameheana na kuwasaidia wale ambao hawana uwezo wa kujisaidia” Sheikh Alhad alisema.

"Tunashukuru sana kwa ushirikiano wenu kwani ndiyo inatupa motisha ya kuendelea kuwapa huduma bora zaidi. Katika shughuli za kuwapa Huduma zilizo bora zaidi na zinazoweza kuwahudumia ukiwa hapa nchini na hata sehemu yeyote duniani. Ningependa pia kuwahakikishia kuwa tutaendelea kuwapa bidhaa bora na kuwasikiliza ili tutimize mahitaji yenu", alisema Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Resolution Insurance Bi Zuhura Muro.


Baadhi ya Watoto yatima, Wafanyakazi wa Multichoice Tanzania pamoja na viongozi wa kituo hicho cha Al-Madina wakichukua chakula katika futari iliyoandaliwa na kampuni ya Multichoice Tanzania.
Baadhi ya Watoto yatima, Wafanyakazi wa Multichoice Tanzania pamoja na viongozi wa kituo hicho cha Al-Madina wakijumuika katika futari hii ikiwa ni moja wapo ya kutoa msaada katika vituo mbalimbali hapa nchini.
Meneja wa Fedha wa Multichoice Tanzania, Francis Senguji akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Kampuni ya Multichoice Tanzania kwa waliofika na kujumuika nao katika futari iliyoandaliwa na Kampuni ya Multichoice Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad