Mlundikano wa Takataka katika Soko la Mchikichini-Ilala jijini Dar es Salaaam ambazo zimekuwa kero kwa wafanyabiashara wa eneo hilo.
Hili ni eneo la kuegesha magari lakini wafanyabiashara wamegeuza kuwa sehemu ya kuuzia bidhaa zao eneo katika Soko la Mchikichini-Ilala jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
wa Soko la Mchikichini-Ilala Jumanne Kongogo akizungumza na baadhi ya
waandishi wa habari waliofika katika Ofisi za Soko la
Mchikichini-Ilala jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na
wafanyabiashara Walemavu kufunga barabara ambayo inaruhusu magari kutoka
na kuingia katika soko hilo, magari ambayo yanatoa huduma katika soko
hilo.
Katibu
wa soko la Mchikichini-Ilala jijini Dar es Salaaam John Andrew
akionyesha takataka zilivyo lundikana katika eneo la soko la
Mchikichini-Ilala baada ya wafanyabiashara kuziba njia inayoruhusu
magari kuingia na kutoka nje ya soko hilo, ambapo hata magari
yanayochukua uchafu katika soko hilo yanashindwa kufika.kuchukua uchafu
huo.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii
Yaani sisi watu weusi, tumefeli kila nyanjaa, yaani mpaka usafi unatushinda, na mahospital duni, dawa hakuna, na hata usafi ziro, hmmmm alafu tunasema tuna Serikali, serikali upupu, Africa kuendelea ni ndoto ikiwa hata mabo madogo madogo tu kama haya ya usafi yanatushinda, tatizo , elimu duni, uaminifu ziro, uongo mwingi, kushinda ukweli
ReplyDelete