Katika katiza katiza za Mtaa kwa Mtaa,nimebahatika kukatiza njia hii ya Mwai Kibaki kama unatokea Mbezi Beach na kukutana na hawa jamaa wenye uwezo mkubwa sana wa kutumia Barabara wakiwa wamepiga mzinga.Kama kawaida yao hawa jamaa,muda wote wanakuwa wanaharaka na hapa hiyo Bajaj ilikuwa ikitokea kwenye njia ndogo kuingia barabara kubwa kulikokuwa na hiyo boda boda.baada ya kushindwa maarifa ya namna ya kukwepana,ndio mambo yakafikia hapa.
Hapo ni mabishano kidogo huku mmoja akitaka alipwe.
No comments:
Post a Comment