Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiwa ndani ya MV Liemba mara walipofika kujionea mandhari ya meli hiyo kongwe duniani.
Nahodha wa MV Liemba, Kapteni Mathew Mwanjisi (Watatu kushoto) akitoa maelezo kwa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.
Nahodha wa Meli ya MV Liemba, Kapteni Mathew Mwanjisi (Kulia) akitoa maelezo ya namna ya kutumia chombo cha kuokolea kwa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango. Wanaomsikiliza ni Kiongozi wa Timu hiyo, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Ufuatiliaji (Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango), Bw. Omary Abdallah.
Mhandisi Mkuu wa Meli ya MV Liemba, Eng. Justine Joachim (Mwenye fulana nyeusi) akiwapa maelezo Wakaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipongia kujionea mitambo ya kuendeshea meli hiyo.
Kazi inaendelea! Watumishi wa Meli ya MV Liemba wakiendelea na kazi ya kushusha shehena ya mahindi kutoka kwenye meli hiyo. PICHA NA SAIDI MKABAKULI
No comments:
Post a Comment