HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 23, 2014

Airtel yatangaza kumi bora wa wiki wa shindano la Airtel Trace Music Stars

Meneja uhusiano wa Airtel Tanzania,Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati alipotangaza washiriki waliongia nafasi ya kumi bora katika mashindano ya Airtel Trace Music Stars kwa wiki hii. Kulia ni Aneth Muga Meneja Masoko wa Airtel Tanzania anaesimamia mashindano hayo ya Airte Trace Music Stars. Hafla ya kutangaza washiriki hao wa 10 bora aimefanyika makao makuu ya Airtel jijini dar es salaam leo.
Meneja Masoko wa Airtel Tanzania,Bi. Aneth Muga akielezea jinsi ya kupiga KURA kwa washiriki waliofanikiwa kuingia 10 bora ya mashindano ya Airte Trace Music Stars. Kulia ni meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando katika hafla ya kuwatangaza washiriki hao iliyofanyika ofisi za Airtel makao makuu morocco Dar es salaam leo.
Mshiriki wa Airtel Trace na moja kati ya 10 bora Karen Gardner akionyeshanamba yake ya ushiriki 55100107 kwa watanzania kumpigia kura.
Mshiriki wa Airtel Trace na moja kati ya 10 bora Christopher kiwele akionyesha namba yake ya ushiriki 55100050 kwa watanzania kumpigia kura.

Mshiriki wa Airtel Trace na moja kati ya 10 bora Jesca charles akiwa pamoja na meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbanod , akionyesha namba yake ya ushiriki 55100135 kwa watanzania kumpigia kura.
Mshiriki wa Airtel Trace na moja kati ya 10 bora John Chambasi akionyesha namba yake ya ushiriki 55100005 kwa watanzania kumpigia kura.
Mshiriki wa Airtel Trace na moja kati ya 10 bora Vanessa Galinoma akiimba na kuonyesha namba yake ya ushiriki 55100232 kwa watanzania kumpigia kura.
Meneja uhusiano wa Airtel Tanzania,Jackson Mmbando (kulia)  na Meneja masoko wa Airtel Tanzania, Bi. Aneth Muga (kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa Airtel Trace Music Stars leo mara baada ya washiriki hao kuongea na waandishi wa habari kwaajili ya kuomba wananchi kuwapigia kura.


Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza washiriki walioingia kumi bora wiki hii katika mashindano ya Airtel Trace Music Stars yenye lengo la kuvumbua na kusaka vipaji vya wanamuziki chipukizi nchini na Afrika kwa ujumla

Shindano hilo lililozinduliwa mwanzoni mwa mwenzi wa Kumi, linaendelea kuwapatia watanzania na wapenzi wa muziki nafasi ya kushiriki kwa kupiga namba 0901002233 na kurekodi wimbo  na kuutuma kisha wimbo huo kutasminiwa na jopo la majaji na kufudhu kuingia katika hatua ya kupigiwa kura .

Akiongea na waandishi wa habari Meneja Masoko wa Airtel Bi Anneth Muga alisema” tunafurahi kuona jinsi gani watanzania wanavyoitikia na kushiriki katika shindano hilo ambapo mpaka sasa limedumu kwa takribani mienzi miwili na nusu. Leo hii tunao wanamuziki chipukizi ambao wameweza kuibuka kuwa katika kumi bora ya wiki hii na tunapenda kuwatangazia jamii, wapenzi wa muziki ili muweze kuwapigia kura na waweze kuendelea kufanya vizuri katika mashindano haya.

Napenda kuchukua fulsa hii kuwakumbusha watanzania kwa Mshindi wa Airtel Trace Music Stars atapatikana kwa vigezo viwili vikubwa  kwanza ni kwa uwezo wake wa kuimba  na pili kutokana na wingi wa kura ,  hivyo tumeona ni vyema sasa kuwaleta kwenu ili muweze kuwawezesha kutimiza ndoto zao  waendelee kwa kuwapigia kura ilie kufanya vizuri kwenye mashindano haya

Kwa upande wake Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alisema “ kwa sasa tuko kwenye hatua muhimu sana ya kuwawezesha washiriki hawa kuendelea mbele kwa kupiga kura, kura yako ndio inahitajika sasa ni rahisi sana  unaweza kupiga kura kwa kupiga namba 0901002233 Kisha ukachagua lugha  na kufata maelekezo, ili kuupigia kura wimbo au mshiriki ni lazima uwe na kodi ya namba yake ya ushiriki hakikisha una kodi namba ya mshiriki unayetaka kuumpia kura wakati wote wa kupiga kura kisha utapata maelekezo ya kuingiza kodi hiyo na baada ya kuingiaza utasikia wimbo wa mwimbaji na kuamua kumpigia kura. Njia ya pili ni kwakuandika ujumbe wenye kodi namba ya ushiriki na kisha kuituma kwenye namba 15594 na tayari utakuwa umepiga kura yako.

Tutaendelea kuwajulisha washiriki watakao ingia kumi bora kila wiki na ili kupata habari hizi kwa urahisi basi tembelea facebook page yetu ya Airtel Tanzania na upata kuona picha za washiriki mbalimbali, namba zao za ushiriki na kusikiliza nyimbo zao kupitia simu yako ya mkononi. Natoa wito kwa watanzania kuendelea kushiriki kwenye mashindano haya kwa kujisajili na kurekodi na kwa kupigia kura washiriki ili tupate mwakilishi bora atakayekwenda kutuwakilisha kwenye mashindano ya Airtel Music Trace Afrika yatakayoshirikisha nchi 17 za Afrika hapo mwaka kesho “ aliongeza mmbando

Akiongea wakati wa maojiano na waandishi wa habari mmoja kati ya washiriki kumi bora wa wiki hii Jesca Charles alisema” najisikia furaha sana kuingia katika kumi bora ya wiki hii, naomba watanzania wanipigia kura kwa wingi ili nisishuke nieendelee kufanya vizuri. Napenda sana kuimba na ndoto yangu ni kuwa mwimbaji wa kimataifa na mwimbaji nae vutiwa nae ni Beyonce natumaini siku moja ntafikia na kuwa mwimbaji nyota kama Beyonce”

Washiriki Walioingia kumi bora wiki hii ni pamoja na Christopher kihwele namba ya ushiriki 55100050, karen Gardner 55100107, Mwinyimkuu Hussein 55100048, John chambasi 55100005, Vanessa Galinoma 55100232, Jesca Charles 55100135, Anne Mkisi 55100004

Mashindano ya Airtel Trace yatafikia kilele mwanzo mwa mwaka kesho ambapo mshindi wa Airtel Trace Afrika atajishindia zawadi kabambe ikiwemo, kurekodi na kusambaziwa nyimbo zake chini ya studio kubwa ulimwenguni pamoja na  safari kwenda nchini marekani na kupata mafunzo ya kimuziki na Nguli wa Muziki wa Amerika Akon

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad