Mkurugenzi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deos Mndeme (kulia), akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiana mkataba wa maelewano ya kibiashara kati ya Taasisi zao. Kushoto ni Ofisa Mkuu wa Mambo ya Ufundi wa Kampuni ya Simu ya Zantel, Moncef Mettiji.
Mkurugenzi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deos Mndeme (kulia) na Ofisa Mkuu wa Mambo ya Ufundi wa Kampuni ya Simu ya Zantel, Moncef Mettiji (kushoto), akimwakilisha Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, wakibadilishana mkataba wa maelewano katika ushirikiano wa kibiashara kwa mambo ya mawasiliano, ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam leo. Katikati ni Meneja Mkuu, Uhusiano na Serikali wa Zanztel, Charles Jutta.
Mkurugenzi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deos Mndeme (kulia) na Ofisa Mkuu wa Mambo ya Ufundi wa Kampuni ya Simu ya Zantel, Moncef Mettiji (kushoto), mwakilisha Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, wakiupitia mkataba wa maelewano katika ushirikiano wa kibiashara kwa mambo ya mawasiliano, mara baada ya kukabidhiana, katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam leo. Katikati ni Meneja Mkuu, Uhusiano na Serikali wa Zanztel, Charles Jutta.
Ofisa Mkuu wa Mambo ya Ufundi wa Kampuni ya Simu ya Zantel, Moncef Mettiji (wapili kulia), akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhiana mkataba wa maelewano ya kibiashara kati ya Taasisi zao. Kulia ni Mkurugenzi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Deos Mndeme.
Baadhi
ya Maofisa wa Kampuni ya Simu ya Zantel, wakiwa katika hafla ya
kukabidhiana mkataba wa maelewano ya kibiashara kati ya Shirika la Posta
Tanzania (TPC) na Kampuni yao hiyo, Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu
Nyerere, Dar es Salaam leo.
Waandishi wa habari wakiwa katika hafla hiyo.
Ofisa Uhusiano wa Shirika la Posta Tanzania (TPC),
Wilifred Miigo, akiwakaribisha wakuu wa Taasisi hizo pamoja na wageni
mbalimbali waliohudhuria katika hafla ya kukabidhiana mikataba ya
maelewano ya kibiashara kati ya Shirika la Posta Tanzania (TPC) na
Kampuni ya Simu ya Zantel, ukumbi wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam leo.(Picha zote na Kassim Mbarouk)
No comments:
Post a Comment