Katika pita pita za hapa na pale kuhakikisha libeneke lenu pendwa la Mtaa kwa Mtaa halilali njaa,niliibuka maeneo ya Tandale kwa mtogole na kukutana na hii ya huyu jamaa wa baiskeli ambaye nae alikuwa akipita katika barabara kubwa kama vionekanavyo vyombo vya moto vikipita,na kilichonistaajabisha kama si kushangaza ni mwendo aliokuwa nao mwendesha baiskeli huyo.ambapo niliona akiyapita magari kibao kama yamesimama vile (na sio kama baiskeli hiyo ina mota,la hashaaa ni uhodari wa jamaa huyo wa kupiga pedeli) kitu ambacho kiliwashangaza wengi katika eneo hilo.
Monday, November 24, 2014
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment