HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 16, 2014

Nani Mtani Jembe awamu ya pili yarindima jijini Mbeya

Wapenzi na mashabiki wa timu mbili za watani wa Jadi Yanga na Simba wakishiriki katika mchezo wa mpira wa meza wakati wa Uzinduzi wa Nani Mtani Jembe awamu ya pili kwenye viwanja vya Kiwanda cha TBL Jijini Mbeya. 
Wafanyakazi wa TBL jijini Mbeya wa ambao ni mashabiki wa Yanga na Simba wakishindana kupiga danadana katika viwanja vya Kiwanda cha TBL Jijini Mbeya.
Mashabiki na wapenzi wa timu ya Simba ambao ni wafanyakazi wa TBL Mbeya wakishangilia ushindi baada ya kuwashinda mashabiki na wapenzi wa timu ya Yanga kwa upigaji wa danadana.
Wafanyakazi wa TBL Mbeya ambao ni wapenzi na mashabiki wa timu za Yanga na Simba wakichuana katika mchezo wa kuvutana kamba kwenye mashindano ya Nani Mtani Jembe kwenye viwanja vya Kiwanda cha TBL.
Meneja wa Bia ya kilimanjaro George Kavishe akielezea mpango wa awamu ya pili wa Bia ya kilimanjaro katika utambulisho wa Nani Mtani Jembe ambayo yanazihusisha timu mbili watani wa Jadi Yanga na Simba.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa timu ya Yanga Mohamed Bhinda akimkabidhi kadi za uanachama Mwenyekiti wa Tawi la Yanga Yohana Samwel kwenye mashindano ya Nani Mtani Jembe kwenye viwanja vya Kiwanda cha TBL jijini Mbeya.
Mmoja wa washiriki wa mashindano ya Nani Mtani Jembe mpenzi wa Simba kwa upande wa wanawake akishiriki katika mashindano ya upigaji Danadana.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad