Na Freddy Macha
Jumatano ijayo tarehe 15 Oktoba, 2014...kundi la kina mama watatu akiwemo Mtanzania litashiriki jopo la ukeketaji na Wabunge, London, Uingereza.
Mtanzania, Rhobi Samwelly, mama wa watoto wanne, ni mzawa wa Butiama, Mara. Wenzake ni Comfort Momoh, toka Nigeria, anayetibu wanawake waliokeketwa hospitali mbili za Guy’s na St Thomas, London na Ann-Marie Wilson mkurugenzi wa “28 Too Many.” Shirika hili lenye tovuti yenye http://28toomany.org/ ni maktaba kubwa yenye habari, picha, utafiti na uchunguzi wa ukeketaji duniani.
![]() |
Bango linalotumika kuchangia makutano na hafla mbalimbali za fedha za ujenzi wa nyumba ya hifadhi ya wasichana Mugumu, Mara |
Mwaka1997 Comfort Momoh alianzisha msururu wa shughuli za kuwasaidia akina mama waliokeketwa likiwemo shirika la African Well Women’s Clinic. Bi Momoh mwenye shahada ya uzamili (MA) ni mshauri wa shirika la Afya duniani (WHO) kuhusu adha ya ukeketaji.
Mtanzania Rhobi na Ann-Marie walikuwa baadhi ya wazungumzaji kwenye hafla iliyofanywa Alhamisi na Jumamosi iliyopita kuchanga fedha za kujenga nyumba ya hifadhi kwa wasichana wanaokimbia ukeketaji, Mugumu, Mara.
No comments:
Post a Comment