Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akimsikiliza Balozi wa
Ujerumani nchini, Egon Kochanke alipokuwa akimfafanulia jambo wakati Balozi huyo na
Naibu wake walipomtembelea Waziri huyo ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, kwa ajili ya
kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Ujerumani na Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kushoto) akiagana na Naibu Balozi
wa Ujerumani nchini, John Reyels wakati Naibu huyo na Balozi wake, Egon Kochanke
(katikati) walipomaliza mazungumzo na Waziri Chikawe ofisini kwake Dar es Salaam baada ya
kujadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Ubalozi huo na Wizara yake. Picha zote
na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.



No comments:
Post a Comment