Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) anawatangazia wananchi
wote kuwa kivuko cha MV. Kigamboni kinatarajiwa kwenda kwenye matengenezo
makubwa wakati wowote kuanzia leo.
Hivyo huduma za uvushaji zitaendelea kwa kutumia vivuko vya MV. Magogoni pamoja
na MV. Lami katika kipindi chote cha matengenezo husika.
Uongozi wa TEMESA unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakao jitokeza.
Kivuko cha MV. Kigamoni
Imetolewa na Ofisi ya Mtendaji Mkuu
TEMESA
23/7/2014
No comments:
Post a Comment