HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 18, 2014

Samsung Tanzania yakabidhi zawadi kwa washindi wake

Mwakilishi wa Kampuni ya Samsung Tanzania, Ibrahim Kombo (kushoto), akimkabidhi jiko la kuokea (Macrowave),Mary Nyarusi mkazi wa Jiji la Arushaambaye ni  mmoja wa wateja walioshinda zawadi mbalimbali baada ya kununua bidhaa halisi za kampuni hiyo,wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi hizo iliyofanyika hivi karibuni kwenye Duka lao lililopo Quality Centre,jijini Dar es Salaam.   
Mwakilishi wa Kampuni ya Samsung Tanzania, Ibrahim Kombo (kushoto), akimkabidhi kamera ndogo ya mfukoni,Mmoja wa washindi hayo,Masimo John ambaye ni Mkazi wa jiji la Arusha aliyeshinda zawadi hiyo.
Mwakilishi wa Kampuni ya Samsung Tanzania, Ibrahim Kombo (kushoto), akimkabidhi Tablet kwa Elizabeth Gasper Mkazi wa jiji la Dar es Salaam,ambaye aliibuka mshindi kwa kununua bidhaa halisi za kampuni hiyo,wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi hizo iliyofanyika hivi karibuni kwenye Duka lao lililopo Quality Centre,jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Kampuni ya Samsung Tanzania, Ibrahim Kombo ( wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa zawadi mbali mbali za Samsung baada ya kuibuka washindi katika promosheni inyaoendeshwa na kampuni hiyo kwa kununua bidhaa halisi za kampuni hiyo,wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi hizo iliyofanyika hivi karibuni kwenye Duka lao lililopo Quality Centre,jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad