HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 25, 2014

SAFARI YA MWISHO YA ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA KALAMBO MKOANI RUKWA NDUGU MOSHI CHANG'A

Baadhi ya Wakuu wa Wilaya nchini na Wananchi wakishiriki kubeba mwili wa Marehemu aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa Hayati Moshi Mussa Chang'a kwa ajili ya kwenda kuusalia katika Msikiti wa Mwanchang'a Kihesa na baadae kupelekwa katika makaburi Mtwivila alikozikwa rasmi na mamia ya wananchi walijitokeza katika msiba huo Mkoani Iringa jana.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Symthies Pangisa akitoa salam zo Ofisi yake katika msiba huo.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mhe. Iddi Kimanta ambae mpaka Marehemu anakutwa na Umauti ndiye aliyekuwa akikaimu nafasi yake ya Ukuu wa Wilaya ya Kalambo akishirikina na Mhe. Venance Mwamoto Mkuu wa Wilaya ya Kibondo kufunua jeneza la Ndugu Chang'a kwa kuondoa bendera ya taifa kuashiria itifaki za Kiserikali kukamilika tayari kupisha taratibu za kidini za kwenda kumpumzisha Marehemu aliyezikwa kwa taratibu za dini ya Kiislamu.
Mamia ya wananchi  wakielekea katika makaburi ya Mtwivila Mkoani Iringa kwa ajili ya kumpumzisha Ndugu Chang'a.
Safari ya mwisho hapa duniani ya Mhe. Chang'a aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo ndio imeishia hapa, wananchi wakishirikiana kuuhifadhi mwili wake katika nyumba yake ya kudumu (kaburi). Kila mmoja ajipime na ajiandae kwa safari hii isiyokwepeka.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akisalimiana kwa majonzi makubwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda mara baada ya kuwasili Nyumbani kwa Marehemu Moshi Chang'a kwa ajili Mazishi. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Hawa Ghasia aliyeiwakilisha Serikali katika Msiba huo mkubwa.
Sehemu ya meza kuu ikitafakari msiba huo kwa majonzi.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akisaini kitabu cha maombolezo, Katika salam zake Mhe. Makinda alimuelezea Chang'a kama mtu muhimu sana katika maisha yake ya siasa kwani mnamo mwaka 1995 akiwa Katibu wa CCM Wilaya ya Njombe alimsaidia sana katika harakati za kisiasa ambazo zimemfikisha hapo alipo hivi leo, Kwa mujibu wa Mama Makinda alisema "...bila ya Chang'a leo hii nisingeitwa Spika....".
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akisoma wasifu wa marehemu ambae ameacha watoto watano; wakiume watatu na wakike wawili na mjukuu mmoja. Katika kumuelezea Ndugu Chang'a Mkuu huyo wa Mkoa alieleza miongoni mwa mambo yatakayomfanya asimsahau chang'a ikiwa ni pamoja na kumuubiri Mungu mara zote katika ziara zake ambapo alitolea mfano kwa kuimba moja ya wimbo aliokuwa akiupenda zaidi wa kumtukuza Mungu wa "KWELI MUNGU WA AJABU" wimbo ambao uligusa hisia za watu na kupelekea kutokwa na machozi ya bila kupenda wakiwepo wanawake na wanaume.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro wakisikitika kwa msiba huo.

(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad