Balozi wa Tanzania Nchini Ujerumani Mhe. Philip Marmo (kushoto) akisisitiza jambo wakati akimkaribisha Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo ( aliyekaa upande wa kulia).
Afisa Mkuu wa Utawala na Fedha katika ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani Bw. Caesar Waitara akifafanua jambo katika kikao hicho.
Baadhi ya washiriki watakaoshiriki maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanyanyika na Zanzibar wakimsikiliza kwa makini balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Philip Marmo (hayupo pichani).
Na Greyson Mwase, Ujerumani
Waziri
wa nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo anatarajiwa kuwa mgeni
rasmi katika kongamano litakalofanyika kesho Berlin nchini Ujerumani
ambapo atawasilisha mada kuhusiana na fursa za uwekezaji nchini Tanzania
hususan katika sekta ya mafuta na gesi.
Kongamano
hilo litakaloshirikisha wasomi mbalimbali litaenda sambamba na maonesho
yatakayooneshwa na wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini kama
moja ya maadhimisho ya jubilee ya miaka 50 ya muungano kati ya
Tanganyika na Zanzibar.
Akizungumza
wakati wa kumkaribisha Prof. Muhongo Ujerumani, Balozi wa Tanzania
nchini Ujerumani Mhe. Philip Marmo alisema kuwa mbali na mada itakayowasilishwa
na Prof Muhongo mada nyingine zitakazowasilishwa ni pamoja na fursa
zilizopo katika sekta ya madini, kilimo, viwanda ikiwa ni pamoja na
utalii, uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na Ujerumani na
nafasi ya lugha ya Kiswahili katika kuimarisha umoja.
Balozi
Marmo aliongeza kuwa maadhimisho ya miaka 50 ya muungano baina ya
Tanyanyika na Zanzibar yatahudhuriwa na wawakilishi kutoka balozi
mbalimbali na watanzania waishio nchini Ujerumani.
Balozi
Marmo aliongeza kuwa katika historia ya nchi ya Tanzania ukoloni
uliacha mambo ya kukumbukwa kama vile miundombinu ikiwa ni pamoja na
mashule na mahospitali.
“Pamoja
na changamoto katika ukoloni lakini umeacha alama za kukumbukwa hususan
katika suala zima la miundombinu. “ Alisisitiza Balozi Marmo.
No comments:
Post a Comment