HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 13, 2013

SHIRIKA LA MAENDELEO CIDA KUPITIA MRADI WA WAZAZI NA MWANA (THE MnW PROJECT) LAKABIDHI SIMU SITINI MKOANI RUKWA KURAHISISHA MAWASILIANO KATIKA VITUO VYA AFYA

Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima akipokea boksi la simu kutoka kwa Bi Safia Telatela ambae ni Mratibu wa Mradi wa Wazazi na Mwana nchini (The WnM Project) kwa ajili ya kusaidia mawasiliano kwa vituo vya afya Mkoani Rukwa katika kupambana na vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga. Jumla ya simu sitini aina ya Nokia zimetolewa katika maeneo ya mradi huo Mkoani Rukwa ambayo ni Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Vijijini, Kalambo na Nkasi. Akizungumza katika hafla hiyo Katibu Tawala Mkoa hu amelishukuru shirika la maendeleo CIDA kwa kufadhili mradi huo utakaosaidia kuokoa maisha ya mama wajawazito na watoto kwa kurahisisha mawasiliano na sehemu zenye huduma sahihi za afya.
Afisa Tawala wa Mradi huo wa Wazazi na Mwana (MnW) Bwana Mashauri Ndebile akionyesha moja ya simu hizo aina ya Nokia kwa waandishi wa habari waliohudhuria katika hafla hiyo ya makabidhiano. Mradi huo unafadhiliwa na Shirika la Maendeleo CIDA na kutekelezwa na Miradi Mitatu ya Plan, Africare, Jhpiego kwa kushirikiana na MOHSW. Mradi huo unatekelezwa katika Mikoa miwili nchini ambayo ni Mwanza kwa Wilaya za Ilemela na Sengerema na Rukwa kwa Wilaya za Kalambo, Nkasi na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Vijijini.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima akizindua simu hizo kwa kupiga simu moja ya majaribio. 
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Ndugu Kimulika Galikunga Boksi moja lenye simu ishirini kwa ajili ya vituo vya afya katika halmashauri hiyo. 
Bi Safia Telatela ambae ni Mratibu wa Mradi wa Wazazi na Mwana nchini (The WnM Project) akizungumza katika hafla hiyo ambapo alisema lengo kubwa la mradi huo ni kuona vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga vinapungua na hatimae kuisha kabisa, alisema hilo litawezekana pale jamii, taasisi binafsi, mashirika ya maendeleo na Serikali zitakaposhirikiana katika kuleta ustawi katika eneo hilo.
Picha ya Pamoja.(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad