HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 28, 2013

WAZIRI NCHIMBI ATOA ZAWADI KWA WAHITIMU WALIOFANYA VIZURI KATIKA MASOMO YAO CHUO KIKUU CHA KILIMO CHA SOKOINE (SUA) LEO

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza na wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine pamoja na wanafunzi waliofanya vizuri karika msomo mbalimbali wanaotarajiwa kufanya mahafali yao kesho tarehe 29, Novemba 2013 katika chuo hicho.  Waziri Nchimbi alitoa vyeti na zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika msomo mbalimbali chuoni hapo. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Gerald Monela. Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Magereza (CGP) John Minja na Makamu Mkuu wa Chuo-Taaluma, Profesa Peter Gillah.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akimpa cheti mwanafunzi Nuru Ally aliyefanya vizuri kuliko wanafunzi wote katika somo la Development Studies katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine kilichopo mjini Morogoro. Mwanafunzi huyo pia alikabidhiwa zawadi ya Shilingi 50,000. Kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo-Taaluma SUA, Profesa Peter Gillah.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wapili kushoto aliyevaa tai) wakiwa katika picha ya pamoja na wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine pamoja na wanafunzi waliofanya vizuri karika msomo mbalimbali wanaotarajiwa kufanya mahafali yao kesho tarehe 29, Novemba 2013 katika chuo hicho.  Waziri Nchimbi alitoa vyeti na zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika msomo mbalimbali chuoni hapo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad