HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 16, 2013

UHABA WA WALIMU WAIKABILI SHULE MOJA MAKETE

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Uganga wilayani Makete akizungumza na mwandishi wetu kuhusu tatizo la upungufu wa waaalimu shuleni hapo.
Mwalimu Yuda Kiluswe ambaye anafundisha darasa la awali hadi la pili akiwa darasani akifundisha.

Edwin Moshi wa Michuzi Media, Makete.

Tatizo la upungufu wa waalimu katika shule mbalimbali wilayani Makete mkoani Njombe limezidi kushika kasi baada ya shule ya msingi Uganga kata ya Luwumbu wilayani hapo kuwa na waalimu wanne tu na wote wakiume licha ya shule hiyo kuwa na wanafunzi wa kike na wakiume.

Tukio hilo la aina yake limedhihirika baada ya mwandishi wa mtandao huu kufunga safari na kwenda shuleni hapo na kuwakuta waalimu hao wakijitahidi kufundisha wanafunzi ambapo jumla ya wanafunzi wote wapo 112.

Mwandishi wetu ameshuhudia mwalimu Yuda Kiluswe ambaye ni mwalimu wa darasa la awali, la kwanza na la pili, akiwafundisha wanafunzi jambo lililomshangaza mwandishi na kwenda kumhoji kulikoni yeye kama mwalimu mwanaume anawafundisha wanafunzi wa darasa la awali hadi la pili ili hali imezoeleka wanafunzi wa madarasa hayo hufundishwa na waalimu wa kike.

Mwalimu Kiluswe amesema analazimika kufundisha madarasa hayo kwa kuwa hakuna mwalimu wa kike shuleni hapo hivyo kulazimu waalimu hao wane waliopo shuleni hapo kufanya kazi zote za kufundisha pamoja na misaada yote wanayohitaji wanafunzi wawapo shuleni hapo.

“Ni kweli imezoeleka wanafunzi hawa wadogo wanafundishwa na waalimu wa kike, lakini kwa kuwa hawapo je tufanye nini, hapa hakuna cha kufanya zaidi ya mimi kuingia darasani na kuwafundisha na wameshazoea na hata mimi pia nimeshazoea” alisema mwalimu Kiluswe.

Akizungumzia suala hilo mwalimu mkuu wa shule hiyo Eliuda Daniel Msigwa amesema ni kweli kuwa shule hiyo ina waalimu wane wote wa kiume wanaohudumia wanafunzi 112 wanaosoma shuleni hapo.

Amesema ni kweli wameshatoa taarifa wilayani kuomba kupatiwa mwalimu wa kike hata mmoja lakini bado kilio hicho hakijasikika hivyo kuiomba halmashauri ya makete kuona namna ya kufanya kuwapa waalimu wa kike hata kwa kuhamisha kutoka shule nyingine na kuwapeleka shuleni hapo.

“Ni kweli tunajua kuwa waalimu hawatoshi lakini mimi ningeshauri, hapa tuna waalimu wanne wakihamisha hata mmoja wa kiume na kumleta mwalimu wa kike badala yake, hii itasaidia wakati tunasubiri serikali kupangia waalimu wengine wapya shuleni hapa” alisema mwalimu mkuu.

Amesema mbali na kuwepo waalimu wanne bado hawatoshi na kusema wakiongezeka angalaua watatu kutawarahisishia kupungua kwa kazi nyingi kwani wanafanya kazi kupita kiasi kutokana na uchache wao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad