HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, August 19, 2013

TIMU YA POLISI YAFIKA SALAMA KATIKA JIJI LA WINDHOEK NCHINI NAMIBIA

Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi,Windhoek Namibia.

Hatimaye timu ya Jeshi la Polisi Tanzania inayoshiriki Michezo ya Nane ya Umoja wa wakuu wa majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika (SARPCCO) nchini Namibia imefika salama na imeanza mazoezi mepesi kwa ajili ya kujiandaa na mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza jumatatu tarehe 19 mwezi Agosti mwaka huu.

Timu hiyo ambayo ni tishio katika michezo hiyo kutokana na historia yake ya ushindi katika mashindano yaliyotangulia imekuwa kivutio kila inapopita huku kila mmoja akitaka kusalimiana nayo.

Timu hiyo inaundwa na wanamichezo 67 ambao wanacheza Mpira wa miguu wanaume, Mpira wa pete Wanawake, Riadha wanaumwe na wanawake na mchezo wa Vishale (Dats).

Michezo hiyo itashirikisha Nchi kumi na nne (14) katika michezo mbalimbali na lengo la michezo hiyo ni kujenga ushirikiano wa Majeshi ya Polisi kwa nchi wanachama wa SARPCCO katika kukabiliana na uhalifu.
timu ya Jeshi la Polisi Tanzania inayoshiriki Michezo ya Nane ya Umoja wa wakuu wa majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika (SARPCCO) nchini Namibia,wakipiga jalamba wakati wa kujiandaa na mashindano hayo.
Timu ya Jeshi la Polisi Tanzania inayoshiriki Michezo nchini Namibia ikiwa kwenye picha ya pamoja na Baadhi ya Wenyeji wao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad