HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, July 29, 2013

LAYLATUL QADIR (USIKU WA CHEO)

Asalaam Alaykum Warahmatu llahi Wabarakatu

Ama Baada ya Salamu naomba toa Shukran zangu za dhati kwako Kaka Michuzi na Timu Nzima ya Blog ya Jamii kwa kutuwekea Ujumbe huu Pili naomba Niwatakie kheri za Mfungo wa Mwezi wa Ramadhani Wadau wote pamoja na timu yako.

Tumuombe M/Mungu azipokee Funga Zetu na Dua zetu kwa Ujumla.

Dhumuni kuu la kuandika Makala hii Nikutaka kukumbushana Siku hii Muhimu katika Siku ambazo Ndio zimeufanya Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani kuwa Mwezi Mtukufu nayo Ni Siku ya LAYLATUL QADIR (USIKU WA CHEO) ambayo ipo katika Kumi hili la Mwisho ambalo tumelianza.

LAYLATUL QADIR (USIKU WA CHEO) NI USIKU AMBAO UNAPATIKANA NDANI YA MWEZI HUU MTUKUFU WA RAMADHANI NDANI YA KUMI LA MWISHO MTUME (S.A.W) LILIPOKUWA LIKIINGIA KUMI LA MWISHO ALIKUWA AKIZIDISHA IBADA KWA SANA NA KUWA AMSHA WATU WAKE ( ALHAL BAYTI ) KWA AJILI YA KUFANYA IBADA ZAIDI KATIKA KUMI HILO.

LAYLATU QADIR SI MWEZI 27 TU ILA WENGI WA WANACHUONI WAMEJITAHIDI KUWA HIYO NDIO SIKU YA LAYLATUL QADIR

SIKU HII HUENDA IKAPATIKANA NDANI YA MWEZI 21 , 23 , 25 , 27 , 29 , NI JUU YETU NDUGU ZANGU KUITAFUTA SIKU HII KWA KUFANYA IBADA KWA WINGI NDANI YA KUMI LA MWISHO ILI M/MUNGU ATUWEZESHE KUIDIRIKI SIKU AMBAYO UBORA WAKE KWA WENYE KUUDIRIKI USIKU HUU KWA IBADA NI ZAIDI YA MIEZI 1000 NA HUSHUKA MALAIKA NDANI YA SIKU HIYO KWA IDHINI YA M/MUNGU NA MALAIKA JIBRIL HUSHUKA.

NI JUU YETU KUHAMASISHANA NAKUKUMBUSHANA KUWA SIKU HII NI SIKU MOJA NA NI MUHIMU SANA ILI KUPATA KUMUOMBA M/MUNGU NA KULIOMBEA TAIFA LETU LA TANZANIA KWA M/MUNGU KUEPUKIKA NA KILA AINA ZA FITNA .

Katika Mambo ambayo yame kokotezwa (Sunnah) katika Kumi hili la Mwisho Ni Kikazi cha Itkafu na Maana ya ITKAFU KI SHAARIA ni Kushikamana na Msikiti na kukaa ndani yake pasina ya kutoka kwa ajili ya kujikurubisha(kuwa karibu) kwa M/Mungu Mtukufu .

Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu ziwe juu yake alikuwa akikaa itikafu katika kila Mwaka ndani ya kumi la mwisho la Ramadhani na Mwaka alio fariki alikaa itikafu muda wa siku ishirini Kama ilivyo pokelewa na Bukhari.

Vile vile Maswahaba wa Mtume na Wake zake walikaa nae itikafu na walikaa Itikafu baada ya mtume kufariki.

M/MUNGU AKIKUBARIKI KUIDIRIKI USIKU HUU WA CHEO SOMA DUA HII KWA MAELEKEZO YA MAMA AISHA alimuliza Mtume Jee? tukiidiriki LAYLATUL QADIR (USIKU WA CHEO) tufanye nini ? Mtume akajibu kithirisha kusema NASH-HADU ANLAA ILAAHA ILLA ALLAHU NASTAGHFIRULLAH NAS'ALUKAL JANNATA WANAUDHUBIKA MINA NNAAR ALLAHUMA INNAKA AFUWUN TUHIBUL AFWAA FA'AFUANNAA YAA KARIYMAL AFWU ". Kama alivyosema Mtume.

MUNGU NDIYE MJUZI WA HII SIKU NI JUU YETU NA FAMILIA ZETU KUZIDISHA IBADA .

Kwa Fikra zaidi fatilia katika Ukurasa wetu wa Facebook : Kijana wa Kiislam Tanzania au ID Fb : Kijana wa Kiislam Dsm Whatsapp :+201110189580

Na:-
Ghalib Nassor Monero l Azhariy.
Al- Azhar University.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad