Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano, Profesa Patrick Makungu (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa kiongozi wa msafara wa wanafunzi toka Chuo cha Uongozi wa Juu wa Kijeshi cha Ghana, Brigedia Jenerali A. Annan jana jijini Dar es Salaam. Wanafunzi hao walitembelea wizara hiyo kama moja ya ziara yao ya mafunzo hapa nchini.
Kiongozi wa msafara wa wanafunzi toka Chuo cha Uongozi wa Juu wa Kijeshi cha Ghana, Brigedia Jenerali A. Annan (Kulia) akiongea wakati ujumbe wake ulipotembelea Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Patrick Makungu na Mkurugenzi wa Sayansi na Teknolojia wizarani hapo Prof. Evelyne Mbede.
Jeshi
la Wananchi wa Tanzania limetakiwa kuendelea kuwa katika mstari wa
mbele katika kuendeleza ubunifu wa kisayansi ili kuharakisha juhudi za
kujiletea maendeleo lenyewe na taifa kwa ujumla.
Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano, Profesa Patrick Makungu
ameyasema hayo alipotembelewa na wanafunzi wa Chuo cha Uongozi wa Juu wa
Kijeshi cha Ghana ambao wapo nchini katika ziara ya mafunzo.
Profesa
Makungu amelitaka jeshi kufanya kazi nyingine zaidi ya kazi zao za
kijeshi ili kuweza kuisaidia nchi na jamii kujiletea maendeleo. “Jeshi
linapaswa kuchukua nafasi ya kwanza kabisa katika juhudi za kuunganisha
bara la Afrika kupitia sayansi na techinolojia,” alisema.
Kwa
upande wake,Mkurugenzi wa Sayansi na Teknolojia katika Wizara hiyo,
Profesa Evelyne Mbede amewakumbusha wanajeshi hao kuwa maendeleo
yaliyopatikana leo katika sekta ya teknolojia ni matunda ya tafiti za
awali zilizokuwa zikifanyika jeshini.
Amelitaka
jeshi la wananchi wa Tanzania kuendeleza moyo wa kukuza teknolojia
kupitia mashirika yake ya Mzinga na Nyumbu ambayo yamekuwa kielelezo cha
wazi kabisa ya jinsi jeshi linavyojihusisha na maendeleo ya sayansi na
teknolojia nchini.
Akiongea kwa niaba ya ujumbe wa wanafunzi
hao,mwambata wa kijeshi wa nchi ya Ghana katika Ubalozi wa Ethiopia,
Brigedia Generali A.Annan, amesema kuwa Afrika kwa sasa inahitaji kuwa
moja kwa kuweza kuunganisha rasilimali na nguvu pamoja ili kuwa na
sauti.
Ameongeza
kuwa ndoto yake ya muda mrefu ni kuona Afrika inakuwa na sarafu moja
huku vikwazo vya kimipaka navyo vikiondolewa ili kuwezesha watu kuvuka
mipaka toka sehemu moja kwenda nyingine. Awali akiwasilisha mada juu ya
jinsi ya kuboresha mahusiano na maendeleo ya afrika kupitia sayansi na
techinolojia.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Utafiti katika wizara hiyo, Bwana Raphael Chibunda amesema
Afrika ina nafasi nzuri ya kutatua matatizo yake pamoja kupitia sayansi
na teknolojia. Amesema nchi kama Rwanda imepiga hatua kubwa kutokana na
kuwepo sera bora za maendeleo pamoja na teknolojia.
Amesema
sayansi na teknolojia vina nafasi kubwa ya kuweza kuboresha maisha ya
watu wa kawaida na kuyafanya yawe bora. Ujumbe huo ulikabidhiwa zawadi
na Profesa Makungu na baadae ujumbe huo uliweza pia kutoa zawadi kwa
Wizara hiyo.
Ni
utaraibu wa kijeshi kwa wanafunzi wake katika kozi za ngazi ya uongozi
wa juu kutembelea nchi mbalimbali ambapo wanafunzi kutoka mataifa
mbalimbali wanapata nafasi ya kutembelea mataifa mengine kwa lengo la
kujifunza. Msafara huo ulijumuisha wanafunzi wa mataifa mbalimbali
wanaoshiriki mafunzo katika chuo hicho. Mataifa hayo ni Ghana,Nigeria,
Rwanda,Tanzania, Mali na Afrika ya kusini.
No comments:
Post a Comment