Pichani ni waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwa katika maandamano ya amani (Picha na Maktaba).
---
Watu wengi kwa sasa wameibuka na kutokea kuipenda fani ya uandishi wa habari bila kujua misingi na miiko ya uandishi wa habari. Tatizo moja ambalo limeonekana ni kubwa sana ni utandawazi ambao umekuwepo na kutokea ibuko la kila kijana kufungua gazeti tando (blog).
---
Watu wengi kwa sasa wameibuka na kutokea kuipenda fani ya uandishi wa habari bila kujua misingi na miiko ya uandishi wa habari. Tatizo moja ambalo limeonekana ni kubwa sana ni utandawazi ambao umekuwepo na kutokea ibuko la kila kijana kufungua gazeti tando (blog).
Hatukatai kuja kwa 
magazeti tando ila naomba tujiulize, yanatumika ipasavyo ama ndiyo 
limekuwa ni wimbi vamizi lenye kutoa ama kusambaza habari hata zile 
zisizokuwa na vyanzo kamili na visivyojitosheleza.Kwa sasa imezuka tabia
 ya wanaojiita wamiliki wa magazeti tando,wengi wao kukopi na kupaste 
vitu wanavyoviokota katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter, facebook
 na mingine mingi.
Sina nia ya kumsema
 mtu bali napenda tuelimishane kama vijana wenzangu,ambao wametokea 
kuipenda fani ya uandishi wa habari, wakumbuke kuwa fani ya uandishi wa 
habari ina miiko na maadili yake, mfano. Katika kuandika habari za 
mazingira, siasa, elimu, uchumi, michezo, burudani ukiangalia habari 
hizi zote zina misingi na miiko yake. Leo hauwezi kumchukua mwandishi wa
 habari za michezo ukamwambia aandike habari za uchumi kwa vile hatakuwa
 na takwimu za uchumi na hata akiandika hiyo habari na kuisoma utakuwa 
unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.
Vile vile ni vizuri
 vijana wenzangu kutambua kuwa kila kazi ina mipaka na misingi yake, 
juzi juzi nilisoma habari katika gazeti tando moja wapo ikisema, 
'ALIYEONGOZA MAANDAMANO YA IRINGA MHESHIMIWA MCHUNGAJI MSIGWA ASWEKWA 
NDANI' nilijiuliza maswali mengi ambayo kiukweli nilikosa majibu yake, 
kuona huyu aliyeandika hiki kichwa cha habari kweli amepitia fani ya 
uandishi wa habari ama ndio ule upepo vamizi?
Maana unapoandika 
habari za mahakamani, polisi kuna misemo yake, hauwezi kumuhukumu mtu 
moja kwa moja kwa kusema fulani ni mwizi, hata hao polisi ambao huwa 
wanakwenda kukamata watu eneo la tukio hawawezi kusema fulani ni mwizi 
mpaka apelekwe mahakamani ndipo sheria ichukue mkondo wake na kumbaini 
huyo aliyekamatwa ni mwizi.
Naomba tufike 
mahali tuheshimu utu wa watu na kuepuka udhalilishaji wa bila kujua 
naamini baadhi ya vijana wengi walioamua kufungua magazeti hayo tando 
ambayo yanatoa habari, hawana taaluma ya uandishi wa habari.
Napenda kuwapongeza
 wale walioamua kufungua magazeti tando katika milengo yao tofauti 
ikiwemo kutoa habari kwa njia ya 'kufundisha masuala ya urembo, mapishi,
 kuwasaidia kuwatangaza vijana katika muziki na hata wale walioamua 
kuandika habari zao binafsi.
Nayasema yote hayo 
kwa vile kumezuka wimbi la vijana wanaotaka kuichafua fani ya uandishi 
wa habari na ionekane si fani ya watu walioenda shule bali ni ya wahuni 
tu wasiojua mambo, naomba vijana tuelimike na tujifunze kwa watu 
wanayoyajua mambo ili tuweze kufika mbele zaidi.
Namalizia kwa kusema tusipoziba ufa tutajenga ukuta.
Asanteni sana kwa kusoma.
Imeandikwa na Cathbert A. Kajuna

No comments:
Post a Comment