HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 19, 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATOA POLE KWA WAFIWA MSIBA WA ASKARI WA USALAMA BARABARANI ALIYEGONGWA NA GARI JANA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa askari wa Usalama Barabarani, WP Elikizaeli Lokisa Nnko, aliyefariki dunia kwa kugongwa na gari na dereva ambaye hadi sasa hajajulikana wakati akiwa katika majukumu yake ya kikazi eneo la Bamaga Mwenge jijini Dar es Salaam jana.
Picha ya Marehemu enzi za uhai wake.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji Prince David, mtoto wa aliyekuwa askari wa Usalama Barabarani, marehemu WP Elikizaeli Lokisa Nnko, aliyefariki dunia kwa kugongwa na gari na dereva ambaye hadi sasa hajajulikana wakati akiwa katika majukumu yake ya kikazi eneo la Bamaga Mwenge jijini Dar es Salaam jana.
Kutoka (kulia) ni Mume wa Marehemu, David Erasto Luharara, watoto wa marehem, Prince David na Abdulhaman David, wakiwa na huzuni.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu kuomboleza msiba huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad