HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 21, 2013

charlz baba na mcd wana mikataba ya kisheria na Mashujaa band

UONGOZI wa Bendi ya Mashujaa Wana Kibega, umesema uvumi wa kuwa Wanamuziki Charles Gabriel 'Chalz Baba' na Sudi Mohamed MCD wanatimka katika bendi hiyo si kweli.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Mkurugenzi wa bendi hiyo Sakina Mbange, amesema kuwa kupanda kwa wanamuziki hao katika jukwaa la bendi nyingine si kama wamehamia huko.

Mbange alisema kuwa kila mtu ana tambua maana ya sheria ambapo mikataba ya hao wanamuziki ipo kisheria hivyo ni mali yao kwa sababu wana mikataba.

"Nina amini kila mtu anatambua nini mana ya sheria wanamuziki wetu wapo kisheria tumewapa mikataba hivyo kama kuna mtu anajaribu kuwashawishi atapata tatizo kubwa"alisema Mbange.

Pia alisema wao hawawezi kumzuia mwanamuziki kupanda jukwaani hivyo wana amini kila bendi ni kama ndugu.

Mbange alisema wanamuziki hao wapo kazini kama kawaida na wanaendelea na kazi zao za kila siku.

Nae Mwamuzi Chalz Baba amewataka mashabiki wa bendi yake wasiwe na shaka na tetesi zilizozagaa kuwa yuko mbioni kutimka na kuamia bendi yake ya zamani ya The African Stars Twanga Pepeta.

Alisema si kweli kama anajiandaa kurejea Twanga Pepeta, alisema ni uvumi tu ambao kuna watu wameamua kuutengeneza.

"Kwanza sina mpango wa kuondoka sehemu ambayo nina amini nipo vizuri kikazi na ninashirikiana na wenzangu kwa moyo mmoja...na nafanya kazi kwa mkataba"alisema Chalz Baba.

Alisema kuna watu wameamua kueneza uvumi huo, wana ajenda ya kuvuruga mshikamano uliopo ndani ya Mashujaa.

“Mimi ni mwanamuziki wa Mashujaa, nina mkataba mrefu na nina uheshimu, bendi yoyote inayonihitaji ni lazima ikae mezani na Mashujaa hakuna njia ya mkato nina amani na maisha ya Mashujaa, natarajia kukaa hapa hadi mwisho wa mkataba wangu” alisema Chaz Baba.

Akifafanua kuhusu kupanda jukwaa la Twanga Pepeta jambo ambalo limezidi kupalilia uvumi wa kuondoka kwake Mashujaa, Chalz Baba alisema kukwea jukwaa la Twanga au bendi nyingine yoyote ni sehemu ya kukaribisha urafiki baina ya bendi yake na bendi zingine. “Hii tunaita kusalimiana kisanii, ni jambo la kawaida sana” alifafanua

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad