Jengo kuu la Ghorofa 5 ambalo lilikuwa halijamalizika ujenzi wake lililopo eneo la Sinza Mori karibu kabisa na Masjid Qubah,limeporomoka jioni hii na kusababisha kifo cha mtu mmoja ambaye alikuwa na wenzake wawili jirani na jengo hilo,ambapo mmoja alivyoona hatari hiyo alikimbia na kuwaacha wenzie wawili ambao walinasa ndani.
Kati ya walionasa mmoja amefanikiwa kutolewa huku akiwa ameumia vibaya na mwingine ndio huyo aliepoteza maisha.
Inasemekana chanzo cha kuanguka kwa jengo hilo la Ghorofa ni hali yake ya kukaa kwa muda mrefu bila kumalizika kwa ujenzi waka ambapo inadaiwa kuwa lina umri wa zaidi ya miaka 10.
Habari kamili itafuata baadae kidogo.

No comments:
Post a Comment