HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 27, 2012

Vodacom yaupa nguvu Mradi wa Mbwa Mwitu

Rais Jakaya Kikwete akionesha mbwa mwitu(hawapo pichani) wanavyorejea katika hifadhi ya Serengeti mara baada ya kuachiwa kutoka katika banda maalum walilokuwa wamehifadhiwa ikiwa ni awamu ya pili ya kundi la mbwa hao chini ya Mradi wa Uhifadhi na Ulinzi wa wanyama hao walio katika hatari ya kutoweka. Vodacom Foundation hadi sasa imeshatumia zaidi ya Sh 450 Milioni kufadhili mradi huo kama sehemu ya kuchangia maendeleo ya sekta ya Utalii nchini. Kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Tifa - TANAPA Allan Kijazi, Meneja wa Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim na Meneja wa Vodacom Foundation Grace Lyon. 
Rais Jakaya Kiwete Kikwete akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani)katika eneo la Nyamuma ndani ya hifadhi ya taifa ya Serengeti mara baada ya kuongoza zoezi la kuwaruhusu mbwa mwitu kumi na watano kurejea hifadhini baada ya kuwa chini ya uangalizi maalum kupitia mradi wa Uhifadhi na Ulinzi wa Wanyama hao walio katika hatari ya kutoweka. Vodacom Foundation hadi sasa imeshatumia zaidi ya Sh 450 Milioni kufadhili mradi huo kama sehemu ya kuchangia maendeleo ya sekta ya Utalii nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad