HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 5, 2012

MABINGWA WA MASHINDANO YA MITUMBWI MWANZA WAPATIKANA.

Msanii wa kikundi cha ngoma cha Bujora akichezea nyoka kwa kuingiza kichwa mdomoni wakati wakitumbuiza watu waliofika kushuhudia mashindano ya mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) yaliyofanyika Mwaloni Mkoani Mwanza jana.

DSC_0208Wapiga makasia 15 wakinyosha makasia yao juu kabla ya kuanza kwa fainali za mashindano ya mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) yaliyofanyika jijini Mwanza jana.
Mabingwa wa Mkoa wa Mwanza wa Mashindano ya Mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) timu ya Cheka na Wengi kutoka Misungwi wakiwasili ufukweni baada ya kuongoza mbio hizo muda wote huku wanaofuatia wakipishana kwa sekunde tu.

Nahodha wa timu ya Chekanawengi ya Misungwi Daniel Mugeng'a, akionyesha kitita cha Tsh 900,000 baada ya kukabidhiwa kutokana na kuibuka mabingwa kwenye mashindano ya Mitumbwi  (Balimi Boat Race) ngazi ya Mkoa jijini Mwanza jana ambapo washiriki walishindana kuendesha  mitumbwi kwa makasia.

Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL Fimbo Butallah, akimuelekeza jambo Nahodha wa timu ya Wanawake na Maendeleo ya Misungwi Tabu Daudi, ambao ndio washindi wa kwanza  kwa upande wa wanawake Mkoa wa Mwanza mara baada ya kukabidhiwa zawadi yao ya ushindi wa kwanza kitita cha shilingi laki saba (700,000).

Mabingwa wa mashindano ya Mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) Mkoani Mwanza  upande wa wanawake timu ya Wanawake na Maendeleo kutoka Misungwi  wakiwa hawaamini kama wameweza kushinda kwa kuwaacha mbali wenzao na  kuwa mabingwa wa mkoa huo na kukabidhiwa jumla ya shilingi laki saba (700,000) kama zawadi ya ushindi wa kwanza.

Wapiga makasia 15 wakinyosha makasia yao juu kabla ya kuanza kwa fainali za mashindano ya mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) yaliyofanyika jijini Mwanza jana.

Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL akiteta jambo na Afisa Utamaduni na Michezo wa Manispaa ya Ilemela  wakati wa mashindano ya Mitumbwi ya Balimi (Balimi Boat Race) Yaliyofanyika jana Mkoani Mwanza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad