HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 13, 2012

KAMERA YA MTAA KWA MTAA MUSOMA MKOANI MARA.

Wachuuzi wa samaki aina ya dagaa wakisubiri wateja kwenye soko la Mwigobero Wilayani Musoma Mkoani mara ambapo walieleza blog hii kuwa bei ya dagaa imeshuka kwa asilimia 50 na zaidi kwa sasa sababu ikielezwa kupungua kwa wateja. Awali bei ya dagaa hao kwa ndoo moja ikiuzwa kwa Tsh 10,000 lakini sasa inauzwa Tsh 5000 hadi 4000.
Mifuko ya Plastic (viroba) inayoonekana imesheheni dagaa hao wakiwa tayari kusafirishwa kwenda maeneo mbalimbali nnje ya Mkoa huo.
Kama ilivyo kwenye mikoa mingi hapa nchini ni kawaida kukutana na watoto wa umri huu mitaanio wakifanya shughuli mbalimbali huku wengine wakiomba omba lakini hapa watoto wengi wapo kwenye ajira hizi za biashara ndogondogo.
MAAJABU YA KAMANGO! Mchuuzi wa samaki wa Soko la Mwigobero Wilayani Musoma akimkata samaki aina ya Kamongo huku samaki huyo akiwa hai na akimuepuka kuto mgusa kichwani kwani pamoja nakuwa amekatwa bado ni mzima na anaweza kukuuma na kukuathiri. Kwa mujibu wa maelezo ya wachuuzi hao samaki huyo ni mgumu kufa hata kama akikatwa vipande vyote lakini kichwa kinakua hai kwa masaa kadhaa bila yakufa na kinaweza kumuuma mtu.
Jengo la Maktaba Kuu ya Mkoa wa Mara lilipo Wilayani Musoma likiwa kwenye hali mbaya ya uchakavu bila ya kukarabatiwa huku likiendelea kutumika kwenye mazingira hayohayo chakavu, baadhi ya maeneo likionyesha kuvuja.
UMEONA TOFAUTI HAPO? Pichani ni wanafunzi wa shule mbili tofauti, kuna Sekondari na Primary lakini wanaonekana kufanana kwa umri lakini pia hawa wa Sekondari ndio waliokuwa wakicheza michezo ya kitoto ya primary kwa kuchota maji taka na kuwarushia wenzao wa primary ! (Ila wote ni watoto).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad