HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 17, 2012

Warembo wa Redd's Miss Tanzania watembelea Mapango ya Amboni jijini Tanga


Washiriki wa Shindano la Redd's Miss Tanzania 2012, hizi karibuni walikamilisha ziara yao ya Kutembelea Mikoa ya Kanda ya Kaskazini ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga kujionea vivutio vya utalii katika mikoa hiyo ambapo walimalizia mkoani Tanga kwa kutmbelea Mapango ya Amboni yaliopo mkoani humo. 

 Warembo hao wakiwa katika mapango hayo ya kale waliweza kujionea vivutio mbalimbali ambavyo ni vya kipekee na vyakuvutia vilivyopo katika mapango hayo ya asili ya zama za kale. Miongoni mwa vitu vilivyopo huko kwenye mapango hayo ni mfano wa sanamu za aina mbalimbali za Bikira Maria, Maandiko ya Quran, Daraja, sanamu za jinsia ya kike na kiume, chui, na vitu vingine mbalimbali vya kuvutia.
Warwmbo wa Redd's Miss Tanzania wakioangalia moja ya vivutio vilivyomo ndani ya Mapango ya Amboni,Jijini Tanga.hapa walikuwa wakionyeshwa mfano wa sanamu ya Mamba.
Warembo wakiwa Nje ya Mapango ya Amboni.
Wakipita katika moja ya Njia za Mapangoni humo.
Sanamu ya Mfano wa Bikila Maria ndani ya Mapango ya Amboni.
Warembo wakimalizia nge ya Mapango hayo.
Vivutio mbali mbali ndani ya Mapango ya Amboni.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad