Historia ya kweli kuhusu ndugu
yetu Upendo Andrew,siku tatu kabla hajatoka masasi girls alipokuwa
amemaliza shule, alitumbukia kwenye shimo lililokuwa likiwaka moto wa
majani makavu ya mwembe, alizama hadi kufikia karibu ya kiuno.
moto
ulikuwa kama umechokolewa na kijiti alipotumbukia, alipelekwa
mkomaindo, na baadaye miguu yake yote miwili ilikatwa, wazazi wake wote
wawili walifariki kabla hatujamaliza shule, baada ya hapo alikuwa
analelewa na babu yake, naye alikuja kufariki so alikosa msaada kabisa
akaamua kwenda dar ambapo hakuwa na ndugu, hivyo akaanza kazi ya omba
omba.
kama
tulivyosikia toka kwa wadau huwa anaomba imala seko na maeneo mengine
ya katikati ya mji, alipata mtu wa kumsomesha compyuta, akapata kazi,
lakini kila akikaa ofisini machozi yanatoka tu hivyo kazi ikashindikana.
aliambiwa na doctor wa hospital ya mission ndanda kuwa kuna mshipa
umefail kichwani ndo unasababisha hayo.
Kwa
maana hiyo alishauriwa kutumia vitamin B, wiki moja kila mwezi, maisha
yake yakawa kimtindo huo, amepanga kigamboni, leo nimempigia simu bahati
nzuri ana simu na anapatikana, Mungu ni wa maajabu, upendo ana mtoto
mdogo wa miezi mitatu, anaishi vipi sasa, mtu aliyemzalisha anafanya
kazi za ndani kwa wahindi, ana mke na watoto wawili, hapa tunaona kabisa
anahitaji msaada mkubwa kutoka kwetu sisi sote, kwani hata shughuli ya
kuomba imesimama kutokana na mtoto ni mdogo, namba yake ni 0715271201.
katika
zungukazunguka yangu na baadhi ya mawazo kutoka kwa watu kwamba je
tumsaidieje kwa kitu cha kudumu, nilimpigia ili kupata mawazo toka
kwake, tuliongea sana akasema basi kama inawezekana akipata computer na
photocopy machine na chuma cha kufanyia biashara hiyo, anaweza kufanya,
sasa wapendwa hebu tujitoeni kwa moyo tufanye tunaloweza ili kumsaidia,
kwa yeyote aliyeguswa either unamfahamu ama humfahamu, lakini taarifa
yake ndo hiyo hapo, amesoma shule ya msingi Ligula iliyoko mkoani Mtwara
na baadae kwenda secondary Masasi Girls.
Kama
umecheza naye hukucheza naye sote ni binadamu sote ni ndugu, kwa
aliyeguswa jamani,Namba ya mpokeaji wa michango ni 0754463508,MRS Anneth
Makunga Ghullam, pia mnaweza kuwasiliana na @violet mkapa on 0754574421
kwa sababu yeye alishawahi kukutana naye ana kwa ana.
Mchango
wako unaweza kufanikisha jambo zima la kumkwamua Dada huyu mwenye
kuhitaji sana msaada wako,kama Mtanzania au mwanadamu yoyote mwenye roho
ya huruma.
Msaada unaohitajika:
Wadau
baada ya kupata historia fupi ya Upendo,msaada unaohitajika ni
wakufanya mpango ili afunguliwe biashara na imekadiliwa milioni mbili
ingeweza kusaidia kufungua biashara hiyo ,mpaka sasa pesa iliyopatikana
ni 460.000,hapo wadau ni mbali mpaka kufikia milioni mbili tu na ndio
maana tunaomba wadau wa sehemu mbalimbali toka mahali popote waweze
kutusaidia kufanikisha jambo hili.
Kutoa
ni moja na pamoja tunaweza fanikisha swala hili zima.Unaweza kujiunga
kwenye kundi hili la kumsaidia upendo kwa Facebook kwa kufuata link hii
hapa http://www.facebook.com/groups/184474061657697/.


kwanza kabisa namuomba mmiliki wa hii page na mtoa mada arekebishe namba ya simu ya Violet Mkapa ni 0754571121
ReplyDelete