HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 31, 2012

REDDS MISS TANZANIA YATANGAZA VIINGILIO NA WASANII


Mkurugenzi wa kampuni ya LINO INTERNATIONAL AGENCY ambao ni waandaaji wa Miss Tanzania,Hashim Lundenga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari juu ya kuanza kuuzwa kwa tiketi za shindano la Taifa la Redd's Miss Tanzania 2012.kushoto kwake ni katibu mkuu wa kamati ya Miss Tanzania, Bosco Majaliwa. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam Mkurugenzi wa kampuni ya LINO AGENCY Hashim Lundenga amesema kuwa,Kutokana na ukubwa wa shindano kwa mwaka huu wale wote watakaofanikiwa kuingia ukumbini watakaa katika viti maalum vilivyowekwa katika hadhi ya kimataifa na kila tiketi itagarimu kiasi cha shilingi laki moja (100,000) za kitanzania.

Kwa upande wa burudani kutakuwa na burudani nyingi sana na zitaongozwa nawasanii nguli hapa nchini kama Diamond Platnum,Winfrida Josephat’Rachel’s pamoja na Wanne star ngoma troupe.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad