HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 12, 2012

NHIF LINDI WALIVYOADHIMISHA SIKU YA AFYA YA AKILI DUNIANI

MAANDAMANO YAKIPITA MBELE YA MGENI RASMI MKUU WA MKOA WA LINDI AMBAYE ALIMWAKILISHA WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII DR.HUSSEIN MWINYI (MB),MH. LUDOVICK MWANANZILA KATIKA SIKU YA AFYA YA AKILI DUNIANI AMBAPO KITAIFA IMEFANYIKA MKOANI LINDI KWENYE VIWANJA VYA ILULU.
KWENYE BANDA LA NHIF MGENI RASMI,MKUU WA MKOA WA LINDI,MH. LUDOVICK MWANANZILA AKITOA RAI KWA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA KUONGEZA KASI YA UHAMASISHAJI WA WANANCHI WA MKOA WA LINDI KUJIUNGA NA CHF,ILI WAPATE UHAKIKA WA MATIBABU.
MWAKILISHI WA NHIF MKOA WA LINDI FORTUNATA RAYMOND AKITOA MAELEZO YA MIKAKATI YA OFISI YAKE KUHUSU MABORESHO YA HUDUMA ZA MATIBABU KATIKA MKOA WA LINDI NA UHAMASISHAJI WA CHF KWA MKUU WA MKOA WA LINDI LUDOVICK MWANANZILA ALIPOTEMBELEA BANDA LA MFUKO HUO KWENYE KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA YA AKILI DUNIANI.
MGENI RASMI AKITIA SAHIHI KWENYE KITABU CHA WAGENI,ANAYESHUHUDIA KUSHOTO NI MENEJA WA NHIF KANDA YA KUSINI JOYCE SUMBWE.


Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ofisi ya Lindi umeshiriki kwenye maadhimisho ya siku ya afya ya akili dunia kitaifa yamefanyika Mkoani Lindi mgeni rasmi ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila ambaye alimwakilisha Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kauli mbiu kwa mwaka huu ni… Sonona Ni Janga La Dunia kwenye viwanja vya Ilulu.

Katika maadhimisho hayo Mfuko umeshiriki kwa kutoa elimu kupitia banda lao kuhusu dhana ya serikali kuanzisha na uratibu wa Mifuko ya Afya ya Jamii (CHF) ili wananchi walio wengi wahamasike kujiunga na pia maboresho ya mafao mbalimbali yanayoendelea kutekelezwa na NHIF kwa wadau na wanachama wake

Mkuu wa Mkoa wa Lindi aliwataka Nhif kujikita zaidi kwenye uhamasishaji zaidi hususani maeneo ya vijijini ambapo mahitaji ya huduma za afya kwa wananchi walio wengi yako huko

…hakikisheni kasi ya uhamasishaji inaongezeka na wanachi  wengi wanajiunga kwenye mfuko huu wa chf,haiwezekani kwa mkoa wa Lindi uwe na  wanachama asilimia 5.4 %   ya kaya 194,424 ,hii ni ishara tosha kuwa wananchi  hawajapata elimu ya dhana na  umuhimu wa mfuko huu katika kupata uhakika wa matibabu,kwani hata kukosekana kwa fedha za  tiba unaweza ukawa chanzo  cha sonona miongoni mwa wanajamii..alisema mkuu huyo wa   mkoa wa Lindi Ludovick Mwananzila

amewataka  mfuko kujipanga vyema kukabiliana na changamoto za huduma za matibabu  zilizopo kwenye mkoa hususani uhaba wa dawa katika vituo vya matibabu,na pale  mtakapohitaji ushirikishwaji wa ofisi yangu kwenye mpango wa uhamasishaji wananchi kujiunga na chf,ofisi yangu iko tayari.alisema Mkuu wa mkoa

akizungumza wakati wa maadhimisho hayo mwakilishi wa ofisi ya Mkoa wa Lindi Fortunata Kulaya alisema changamoto kubwa iko kwenye matumizi ya fedha za tele kwa tele na zinazolipwa na nhif kutokutumiwa kwa malengo yaliyokusudiwa hivyo kudhoofisha mwitikio wa wananchi kujiunga na chf.

Mfuko umekuwa kwenye mkakati wa kuzishauri kamati na bodi za  afya zilizopo kwenye hospitali za mkoa,wilaya na vituo vya kutolea huduma za matibabu kwa halmashauri zote zilizopo mkoani lindi,kuibua vyanzo mbadala vya kununua madawa kupitia malipo ya tele kwa tele  ili wananchi wanapohitaji huduma hiyo ipatikane papo hapo.alisema kulaya

Alisistiza  utaratibu usambazaji dawa uliopo una changamoto zake lakini pia mfuko umeweka utaratibu wa mikopo ya vifaa tiba na ukarabati wa majengo ili halmashauri zikope kwa kuboresha huduma kwenye maeneo hayo.

Pia aliwataka wananchi kuunga mkono juhudi za serikali katika kuhamasisha wananchi kufahamu vyema madhara yanayosababisha sonona kwani tutakuwa tunajenga taifa lisilokuwa na wabunifu wa maendeleo kwani afya ya akili ni ya msingi na kila mwanajamii lazima awe nayo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad