HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 3, 2012

Mpango wa Kuifufua timu ya Tukuyu Stars wapamba moto,Waelekea Mbeya kwenye Kongamano la Kuifufua upya

 Wadau wa timu ya Tukuyu Star Banyambala ya Mbeya wakiwa tayari kwa safari ya kuelekea Tukuyu kwa ajili ya Kongamano la Kuifufua upya timu hiyo iliyovuma miaka ya 1980 na 1990 katika soka la Tanzania na ilifanikiwa kuchuka ubingwa wa Bara mwaka 1986. katika picha kulia ni Kocha Kenny Mwaisabula Mzazi wa pili kutoka kulia waliosimama  ambaye ndiyo kiongozi na Makamu mwenyekiti wa Tukuyu Star Family, Fullshangweblog itakuwa ikikumuvuzishia moja kwa moja matukio ya kongamano hilo kutoka mjini Tukuyu Kesho. yakirushwa na Kamanda wa Fullshangweblog John Bukuku
Hapa wadau hao wakipozi kwa picha kabla ya uanza safari hiyo maeneo ya Ubungo jijini Dar es salaam.
Tayari Wadau wa Tukuyu Star Family wameshawasili hapa Msamvu kwa Bi Mkora wa Maggid Mjengwa mjini Morogoro wanapata chakula cha mchana kabla ya kuendelea na safari yao kuelekea Tukuyu Mkoani Mbeya kwa ajili ya kongamano la kufufua timu ya Tukuyu Star kesho mjini Tukuyu.
Kocha Keny Mwaisabula Mzazi ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Tukuyu Star Family akipata menyu yake kushoto kwa ke ni mchezaji wa zamani Willy Martin na wadau wengine.
Wadau wakiendelea kupata Menyu katika hoteli ya Makuti Msamvu mjini Morogoro.
Kutoka kulia ni Mdau Edward Mwakajinga, Moses Mkandawile na Peter Mwambuja wakisubiri kupata menyu yao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad