HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, July 19, 2012

RAIS KIKWETE NA MAMA SALMA WATUA ZANZIBAR KUFARIJI WAHANGA WALIOPATWA NA AJALI YA MELI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Uwanja wa Maisara, Zanzibar, ambako ndiko miili ya marehemu huletwa kwa utambuzi baada ya kuokolewa kwenye eneo la ajali leo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji mmoja wa wahanga walionusurika katika ajali ya meli jana huko Chumbe wakati Rais na Mama Salma Kikwete walipowatembelea kuwafariji na kuwapa pole katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja leo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa kwenye Uwanja wa Maisara, Zanzibar, wakiangalia miili ya marehemu baada ya kuokolewa kwenye eneo la ajali ya Meli iliyotokea jana karibu na Kisiwa cha Chumbe.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji mmoja wa walionusurika katika ajali ya meli jana huko Chumbwe wakati Rais na Mama Salma Kikwete walipowatembelea kuwafariji na kuwapa pole katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja leo.
Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete wakimsikiliza mmoja wa walionusurika katika ajali ya meli jana Bw Kitwana Makama Haji ambaye kalazwa katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja leo.
Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete wakimpa pole Bi Salome Abeli, mmoja wa walionusurika katika ajali hiyo ya meli. Yeye ni mfanyakazi wa Tanzania Automic Energy Commission akitokea Arusha kwenda Pemba Kikazi leo.PICHA NA IKULU.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad